Na NOEL SYLIVESTER-Mahakama, Songea
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abas Ahmed amewahimiza
Wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Sheria ili kupata elimu ya
sheria kwenye masuala mbalimbali.
Mhe. Ahmed alitoa rai hiyo kwenye uzinduzi wa maadhimisho hayo
yaliyofanyika katika Viwanja vy Soko Kuu Songea.
Mkuu wa Mkoa alibainisha kuwa Wananchi wengi
wanauhitaji na changamoto ya kujua sheria mbalimbali, kama za ndoa, ardhi,
mirathi, hivyo ni vema wakajitokeza katika maadhimisho hayo kwani elimu ya sheria itakayotolewa na Mahakama na Wadau itakuwa bure.
Aliongeza
kuwa kwa mwaka 2025 Mahakama kwa kushirikiana na Wadau watatembelea maeneo mbalimbali na
kutoa elimu bure na msaada
wa kisheria kwa Wananchi katika Shule
za Sekondari na Msingi, Mabaraza ya Usuluhishi, Mabaraza
ya Ndoa, Sokoni, mikutano
ya hadhara na katika radio.
“Ninatoa wito kwa
wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kutumia Wiki ya Sheria kujitokeza
kwa wingi kujua sheria mbalimbali za ndoa, ardhi na kupata msaada wa kisheria
bure,”alisema.
Awali akitoa taarifa
ya maadhimisho hayo, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Songea, Mhe.James Karayemaha
alisema kuwa Wiki ya Sheria inalenga kutoa elimu
ya sheria kwa wananchi kwa kuwafuata katika maeneo
mbalimbali kama mikutano ya hadhara, katika Taasisi
za umma kama shule, vijiwe vya bodaboda, mama ntilie pamoja na wahudumu
wa bar.
Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya Wiki na Siku ya Shweria inasema, “Tanzania 2050: Nafasi ya Taasisi Zinazozimamia Haki Madai katika Kufikia Malengo Makuu ya Dira ya Taifa ya Maendeleo.”
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Songea, Mhe James Karayemaha akisalimia Wananchi kwenye uzinduzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Sheria mkoani Ruvuma.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abas Ahmed akizungumza kwenye uzinduzi huo.
Jaji wa Mahakama Kuu Songea, Mhe Emmanuel Kawishe(katikati).
Jaji Mfawidhi akiwa na Mkuu wa Mkoa pamoja na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu
Songea wakishiriki matembezi kuelekea Viwanja vya Soko Kuu Songea.
Matembezi kuelekea Soko Kuu Songea.
(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dar es Salaam)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni