Na EVELINA ODEMBA – Mahakama, Morogoro
Maelfu
ya Wananchi wamejitokeza kushuhudia uzinduzi wa Wiki ya Sheria ambao kwa Kanda
ya Morogoro ulifanyika kwenye Viwanja vya Stendi ya Daladala ya zamani iliyoko
Morogoro Mjini.
Uzinduzi
huo ulihudhuliwa na Viongozi mbalimbali wa Mahakama na Serikali wakiongozwa na Mkuu
wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Mussa Kilakala aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa
Morogoro.
Akizungumza
wakati wa uzinduzi huo, Mhe. Kilakala, ambaye alikuwa Mgeni Rasmi alisema kuwa amefarijika
kwa uwepo wa Maadhimishi ya Wiki ya Sheria na kutoa rai kuwa suala la
unyanyasaji wa kijinsia lipewe kipaumbele kikubwa wakati wa zoezi la utoaji
elimu.
“Nimefurahi
kusikia kuwa wakati wa Wiki ya Sheria Wananchi watapewa elimu juu ya ukatili wa
kijinsia na ukatili dhidi ya watoto, masuala haya yamekuwa ni tatizo kubwa sana
kwa Mkoa wa Morogoro,” alisema.
Aliwaomba Wananchi wa Mkoa huo kuitumia vyema fursa
hiyo kufika kwenye mabanda ili kupata uelewa juu ya masuala hayo na mengine
mengi yanayohusu sheria.
Jaji
wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Latifa Mansoor, ambaye alihudhuria ufunguzi huo
alisema kuwa katika Wiki ya Sheria mkoani Morogoro wamejipanga kuwafikia Wananchi
mbalimbali.
Alitoa
wito kwa wote ambao wamekuwa na shida mbalimbli za masuala ya kisheria na
hawafahamu namna ya kuifikia Mahakama wafike katika mabanda ili waweze
kutatuliwa shida zao na kupatiwa elimu.
Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro, Mhe. Pascal Kihanga alipalilia suala la Wananchi kuitumia vyema nafasi ya Wiki ya Sheria kwa kuwa wakati mwingine wanapata changamoto ya kuwafikia wanasheria ili kupata ushauri wa masuala yanayohusu sheria.
Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Latifa Mansoor akizungumza wakati wa uzinduzi huo.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro, Mhe. Pascal Kihanga akizungumza wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Sheria.
Watumishi wa Mahakama Kanda ya Morogoro (juu na chini) wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa uzinduzi huo.
Burudani ya ngoma za asili ikiendela katika shamla shamla za uzinduzi wa Wiki ya Sheria Kanda ya Morogoro.
Matukio mbalimbali wakati wa uzinduzi.
(Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dar es Salaam)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni