Jumapili, 26 Januari 2025

SONGWE YAZIDUA WIKI YA MAADHIMISHO YA SHERIA NCHINI

 Na Imani Mzumbwe – Mahakama, Songwe

Hakimu Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Songwe Mhe, Francis Kishenyi jana tarehe 25 Februari, 2025 aliongoza matembezi ya ufunguzi wa maadhimisho ya Wiki Sheria Mkoa wa Songwe na kutoa rai kwa wananchi kuitumia wiki hiyo kupata elimu ya masuala mbalimbali ya kisheria ili jamii ifahamu Mahakama inatoa humama gani kwa jamii.

Akizungumza katika uziduzi huo Mhe. Kishenyi alisema kuwa wiki ya sheria nchini ni fursa pekee kwa Mahakama kushirikiana na wadau wake katika kujadili changamoto na mafanikio katika mfumo wa kisheria lakini pia aliongeza kuwa, wiki ya sheria kutakuwa na mambo mengi ya kuyafanya kama kutoa elimu kwa wananchi katika maeneo mbalimbali kama vile Stendi, Sokoni, Mashuleni na Mahakama ya Hakimu Mkazi Songwe.

Naye, Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa Songwe Bi. Farida Mgomi ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ileje akiwahutubia wananchi amesisitiza na ktoa rai kwa wananchi wa Wilaya ya Mbozi na Mkoa wa Songwe kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho ya wiki ya sheria nchini. Aidha, ameeleza kuwa hiyo ni fursa pekee ya wananchi hao kupata nafasi ya kujifunza mambo ya kisheria na taratibu mbalimbali pamoja na kujua haki zao za msingi hususani haki madai.

Mhe, Farida ameziomba Taasisi mbalimbali kuisaidia Mahakama katika kutoa elimu na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabiri wananchi, Vilevile, Bi. Farida alisema kuwa Taasisi mbalimbali na Mahakama wanatakiwa kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu na uwajibikaji wa hali ya juu wakizingatia misingi ya Usawa, Utawala bora na Haki kwa wote.

“Naomba kutoa rai na kuwaasa wananchi na pia kuwasisitiza kutojichukulia sheria mkononi badala yake wazitumie Mahakama zetu kwani kujichukulia sheria mkononi ni kosa kisheria na kunaweza kusababisha Visa, Hila na Mauaji mbalimbali yasiyo kuwa na sababu kwani jamii iliyostaarabika inafuata taratibu za kisheria,” ameongeza Bi.Farida

Naye, Mtendaji wa Mahakama Mkoa Songwe Bw. Sosteness Mayoka amewashukuru sana Wadau, Watumishi  na Wananchi mbalimbali kwa kujitokeza katika ufunguzi wa wiki sheria Mkoa wa Songwe na amewakaribisha kuendelea kujitokeza katika maeneo mbalimbali  yaliyopangwa kutoa elimu kwa wananchi hao ikiwa ni pamoja na eneo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Songwe.

Katika matembezi hayo wadau na Taasisi mbalimbali zilijitokeza kama vile Ofisi ya Mashtaka Taifa Mkoa wa Songwe, TAKUKURU, Police Mkoa, Uhamiaji Mkoa, Jeshi la Zimamoto, Ofisi ya Ardhi Mkoa, Ustawi wa Jamii, Huduma kwa Jamii, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mawakili wa kujitegemea (TLS).  Matembezi hayo yalianzia Mahakama ya Mwanzo Vwawa Mjini kupitia njia ya NMB hadi viwanja vya Stendi ya Malori Vwawa Mjini.

Hakimu Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Songwe Mhe, Francis Kishenyi akiwahutubia wananchi wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya sheria nchini jana tarehe 25 Januari, 2025

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa Songwe Bi. Farida Mgomi ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ileje akiwahutubia wananchi

Meza Kuu ikiwa inatoa heshima wakati wa wimbo wa Taifa wakati wa maadhimisho ya Wiki Sheria Mkoa wa Songwe.

Sehemu ya wananchi waliohudhulia hafla ya maadhimisho ya Wiki Sheria Mkoa wa Songwe.

Sehemu ya watumishi wa Mahakama waliohudhulia hafla ya maadhimisho ya Wiki Sheria Mkoa wa Songwe.


















Hakuna maoni:

Chapisha Maoni