Jumanne, 28 Januari 2025

MAHAKAMA YAPONGEZWA KWA KUSAMBAZA UPENDO MTAANI

Na INNOCENT KANSHA-Mahakama, Dodoma

Mahakama ya Tanzania imepongezwa na wananchi waliotembelewa mtaani na kupewa elimu ya masuala ya kisheria na kuiomba Mahakama isiishie kutoa elimu katika wiki ya sheria pekee bali ifanye hivyo mara kwa mara hasa maeneo ya vijijini.

Akitoa maoni juu za zoezi la utoaji elimu ya kisheria mtaani Mkazi wa Nkuhungu jijini Dodoma Bw. Juma Issa amesema, Mahakama imepiga hatua kubwa katika kuhudumia wananchi kwani zamani hatukuzoea kuiona Mahakama ikijishughulisha katika mambo hayo ya kutoa elimu mtaani ili ni jambo la kupongeza linapaswa kuigwa na Taasisi zingine za kiserikali.

“Nawapongeza Mahakama na Wadau wake kwa kutoa elimu nzuri kama hii tuliyoipata hapa leo kwani, wengine walikuwa hawafahamu wala walikuwa hawajui lakini leo kupitia gari la matangazo na elimu likiwa na wanasheria wakuu tumejifunza mambo mengi sana na kufahamu mambo mengi sana tuliyokuwa hatuyajui kwa hiyo tunashukuru sana muendelee kutembelea Mkoa wa Dodoma kuwasaidia wale ambao hawajui wapate fursa ya kujua taratibu mbalimbali za uendeshaji wa shughuli za kisheria waendelee kujua na kuzitambua taratibu hizi asanteni sana,” amesikika akisema Bw. Issa.

Naye, Mkazi wa Nkuhungu jijini Dodoma, Bi. Sada Salum Yoram amesema, “nimejisikia furaha sana kuona Mahakama imeleta watu wa kutupata elimu ya sheria kupitia wataalum hawa, kwani kuna wakati unaweza kuwa na haki ukakosa haki na kuna wakati unaweza kuwa huna haki ukapata haki. Mambo ya aina hii ndiyo Mahakama na wadau wake wanapaswa kuyazingatia kwa umakini mkubwa ili wenye haki wasipoteze haki zao…

kuna uwezekano wazazi wetu wamezaa matumbo mengi na tofauti tofauti unakutana na sintofahamu nyingi mtoto wa mwisho anapata mali nyingi anakuzidi wewe uliyemtanguliwa kuzaliwa. Kitu kingine hata kama mzazi akiwa muwazi akisha toweka duniani lazima ndugu wa marehemu watoe maamuzi bila kukusikiliza wewe mtoto mkubwa,” amefafanua Bi. Sada.

“Nimejifunza kitu kikubwa sana na naishukuru sana Mahakama ya Tanzania kwa sababu kuna mambo ambayo nilikuwa siyajui kwa mfano; nilikuwa sijui masuala ya ndoa, kwani zamani nilijua ili mtu aachane na mweza lazima awe amefunga ndoa kisheria ya kiserikali au ya dini, lakini sheria inaelekeza kuwa kuna ndoa ya dhana ambayo uhalali wake ni kuishi pamoja kwa kipindi cha miaka miwili hiyo kisheria inahesabika kama ndoa halali kisheria. Na pia ili ndoa itenguliwe ni lazima muishi pamoja kwa miaka miwili ili Mahakama iweze kuwatenganisha haya yote nimeyapata kupitia elimu hii.  Hili ni jambo kubwa bila Mahakama kuleta elimu hii mimi ningekuwa bado nipo gizani nawapongeza Mahakama ya Tanzania,” ameongeza Bi. Sada.

Akitoa elimu Soko la Mavunde Changombe na Majengo Stendi ya Nkuhungu jijini Dodoma kwa wananchi juu ya masuala ya kisheria kuhusu wosia. Hakimu Mkazi Mhe. Sifa Jacob amesema, Wosia ni maelekezo ambayo mtu anayaacha juu ya namna mali zake alizozichuma zitakavyosimamiwa pale mauti itakapo mkuta.

Aidha, Mhe. Jacob amesema, kuna aina kadhaa za wosia kama vile wosia wa mdomo ambapo mtu anaeleza mali zake zitasimamiwa na nani na zitasimamiwa vipi au zitagawanywa kwa nani na warithi wa mali hizo ni akina nani. Vilevile kuna wosia wa maadishi unaotanabaisha mali za muhusika ni zipi na nani atarithi na zitasimamiwa na nani.

Mhe. Jacob amesema, wosia wa maadishi ni lazima uwe umeshuhudiwa na watu wasiopungua wawili na wosia wa mdomo ni lazima uwe umeshuhudiwa na watu wasiopungua wanne lakini  kama wosia wa maadishi umeandikwa na mtu asiyejua kusoma ni lazima uwe umeshuhudiwa na watu wasipungua wanne ambao wanajua kusoma na kuandika kwa usahihi.

Vilevile, mambo mengine ya msingi ya kuzingatia kwenye wosia Mhe. Jacob amesema, ni kuzingatia vitu gani vinaweza kubatilisha wosia kwani wosia unaadikwa ili kuja kuwa na manufaa baadae kwa hiyo kuna vitu lazima mwandishi wa wosia azingatie ili wosia wake uwe na tija. Mosi ni lazima wosia umtaje waandishi wa wosia husika na huyo mwandishi wa wosia ni lazima awe mtu mzima na mwenye akili timamu awe na umri wa zaidi ya umri wa miaka 18 lakini pia ni lazima awe na akili timamu, awe ameandika wosia huo bila kushurutishwa na mtu yoyote.

“Mtoa wosia lazima ataje kwenye wosia husika mali anazotaka kuzirithisha lakini pia ni lazima ataje warithi wa mali hizo na mwisho asaini wosia huo, lakini kama hajawahi kusoma na kuandika ataweka alama ya dole gumba kuonesha kuwa nyaraka hiyo ni yake na mwisho kabisa wosia ni lazima uwe na tarehe ambayo umeandikwa,” amesisitiza Hakimu Mkazi huyo.

Aidha, Mashariti hayo yasipozingatiwa Mhe. Jacob amesema, wosia huo unaweza kuonekana ni batili mbele ya macho ya kisheria. Lakini jambo lingine la kuzingatia ni wapi mtu anaweza kutunza wosia. Wosia unaweza kutunzwa katika Ofisi za Vizazi na Vifo (RITA) na pia RITA wanaweza kumsaidia mwandishi wa wosia kuandika wosia wenyewe, Ofisi ya Wakili unayemwamini, ndugu unayemwamini au shahidi aliyeshuhudia huo wosia, unaweza kutunza Benki au hata kanisani unakoabudu kama inawezekana.

Mhe. Jacob ameongeza kuwa, kuna faida nyingi za kuandika wosia kwanza kabisa unamuelekeza mwandishi nani atasimamia mirathi hiyo, nani atasimamia pindi mauti inakukuta, moja ya jambo ambalo linasumbua sana baada ya mtu kufariki kwenye utambuzi wa nani mwenye sifa na vigezo vya kusimamia mirathi ni nani asimamie mali za marehemu.

“Kuna watu wanafikira potofu wanafikiri akiwa msimamizi wa mirathi atakuwa mmiliki wa mali hizo au kwa namna yoyote atafaidika na mirathi wanang’ang’ania kusimamia mirathi. Lakini kingine wosia unamuwezesha mwandishi kutaja mali zake na kubainisha ni nani atarithi mali hizo, hivyo muhusika anaweza kutaja mali zake na kuondoa ugomvi wa watu wanaojikweza kuwa warithi halali wa mali za marehemu au ni watoto wa marehemu au ndugu wa marehemu wa karibu wosia unaondoa huo mkanganyiko,” ameongeza Mhe. Jacob.

Faida nyingine aliyoisema Mhe. Jacob ya kuandika wosia ni kulinda undugu wa wanafamilia atakao waacha marehemu baada ya kifo chake na kuondoa sintofahamu miongoni mwao na kuepusha tabia zisizofaa kama vile kupora mali za marehemu na hata kutoana uhai, kutiana uchizi bila sababu bila sababu za msingi.

Mahakama kijiwe nongwa cha kawahawa  Chang'ombe jijini Dodoma elimu ikitolewa kwa wananchi.

Afisa zima moto wa Jeshi la zima moto akitoa vipeperushi kwa wananchi waliofika kwenye gari la kutoelea elimu ya wiki ya sheria jijini Dodoma.










Mama Mjasiliamali soko la Mavunde Mang'ombe jijini Dododma akipitia kwa makini kipeperushu cha elimu ya masuala ya sheria 


Afisa zima moto wa Jeshi la zima moto akitoa vipeperushi kwa wananchi walotembelewa kwenye soko la Mavunde Chang'ombe ikiwa ni sehemu ya kutoa elimu ya wiki ya sheria jijini Dodoma.


Afisa wa Mahakama akimwelimisha mwananchi na kumpatia vipeperushi vya elimu mwananchi wakati wa utoaji elimu ya sheria mtaani.


Mahakama kijiwe nongwa cha kawahawa  Chang'ombe jijini Dodoma elimu ikitolewa kwa wananchi.

Mahakama kijiwe nongwa cha kawahawa  Chang'ombe jijini Dodoma elimu ikitolewa kwa wananchi.







Afisa wa Mahakama akimwelimisha mwananchi na kuwapatia vipeperushi vya elimu mwananchi wakati wa utoaji elimu ya sheria mtaani.

Afisa wa Mahakama akimwelimisha mwananchi na kuwapatia vipeperushi vya elimu mwananchi wakati wa utoaji elimu ya sheria mtaani.

Maafisa wa Mahakama akimwelimisha mwananchi na kuwapatia vipeperushi vya elimu mwananchi wakati wa utoaji elimu ya sheria mtaani.

Mwananchi akisoma chapisho lililoandaliwa na Mahakama kwa ajili ya kutoa elimu ya kisheria mtaani jijini Dodoma.
 
Mwananchi akisoma chapisho lililoandaliwa na Mahakama kwa ajili ya kutoa elimu ya kisheria mtaani jijini Dodoma.

Mwananchi akisoma chapisho lililoandaliwa na Mahakama kwa ajili ya kutoa elimu ya kisheria mtaani jijini Dodoma.

Mwananchi akisoma chapisho lililoandaliwa na Mahakama kwa ajili ya kutoa elimu ya kisheria mtaani jijini Dodoma.


Mwananchi akisoma chapisho lililoandaliwa na Mahakama kwa ajili ya kutoa elimu ya kisheria mtaani jijini Dodoma.



Mwananchi akisoma chapisho lililoandaliwa na Mahakama kwa ajili ya kutoa elimu ya kisheria mtaani jijini Dodoma.

(Picha na Innocent Kansha - Mahakama)

        

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni