Jumapili, 26 Januari 2025

WANANCHI WAITIKIA WITO JIJINI MBEYA KUPATA HUDUMA ZA KISHERIA

Na Daniel Sichula – Mahakama, Mbeya

Kufuatia uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki Sheria, wakazi wa jiji la Mbeya na viunga vyake wajitokeza kwa wingi kupata huduma mbalimbali kutoka kwa Taasisi zinazotoa huduma na elimu ya kisheria katika viwanja vya stendi ya mabasi Kabwe jijini hapo.

Aidha, katika Banda la Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya limepokea wananchi wa rika tofauti tofauti waliokuja kwa lengo la kupata elimu za Mirathi, migogogro ya ardhi, ndoa na baadhi walitaka kujua shughuli na muundo wa Mahakama na namna unavyofanya kazi kwa kushirikiana na Taasisi zingine ikiwemo Mabaraza ya Ardhi.

Wakati huo huo,  wananchi walifika katika mabanda ya wadau wa Sheria na Taasisi za Serikali wakiwemo RITA, Polisi Jamii na Jeshi la Magereza kupata elimu na kupata huduma za usajili wa uzazi na vifo kutoka ofisi ya RITA bila kusahau Taasisi zisizo za Serikali kama vile Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) pamoja na Chuo Kikuu cha Katoliki Mbeya (CuOM) Kitivo cha Sheria na kuonyesha kuwa mstari wa mbele kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi walifika katika viwanja vya stendi ya mabasi Kabwe kupata elimu ya sheria

Aidha, Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC Taifa) walifika kwenye Banda la Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya kwa ajili ya kutoa fursa ya kujua nini kinafanyika kwenye maadhimisho hayo ya Wiki ya Sheria na kuwapa fursa wananchi kujua ni kitu gani watapata wakifaka kwenye viwanja vya stendi ya mabasi kwa ajili ya kupata elimu.

Nao Maafisa Mahakama kama vile Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu, Hakimu Mkazi Mhe. Ayubu Shellimo na Hakimu Mkazi Mhe. Asha Njovu wakihojiwa na Shirika la Utangazaji Tanzania TBC Taifa Mbeya walifafanua kwa undani nini kinafanyika kwa wiki nzima ya maadhimisho ya wiki sheria hadi siku ya kilele pamoja na kuendelea kuwakaribisha wananchi kufika kwa ajili ya kupata elimu ya sheria kutoka Taasisi mbalimbali.

Baadhi ya wananchi walifika walishuruku kwa huduma na elimu mbalimbali zinatolewa “Tunashukuru sana Uongozi wa Mahakama Mbeya kwa mualiko wa Taasisi mbalimbali zilizopo hapa kutoa msaada na elimu ya sheria kwani huduma imetufikia kirahisi kabla tulikua hatujui hata tutawafikia vipi kwa kuwa ofisi zao na hata huduma wanazotoa tulikua hatuzijui,” alisema mmoja wa mkazi wa Mbeya.

Mwandishi wa Habari kutoka TBC Taifa akipata maoni kutoka kwa mwananchi alietembelea mabada ya kutolea elimu kwenye maadhimisho hayo.

Wananchi wakipata huduma kwenye Banda la Chuo Kikuu cha Katoliki jijini Mbeya

Wananchi wakipata huduma kwenye Banda la Rita


Wananchi wakipata huduma katika Banda la Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya

Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu akitema madini mbele ya Mwandishi wa Habari kutoka TBC Taifa.

Hakimu Mkazi Mhe. Asha Njovu wakihojiwa na Shirika la Utangazaji Tanzania TBC Taifa 

Hakimu Mkazi Mhe. Ayubu Shellimo akitoa elimu kwa mwandishi wa habari kutoka TBC Taifa







Hakuna maoni:

Chapisha Maoni