Jumanne, 4 Februari 2025

JAJI DKT. MASABO AFUNGUA MAFUNZO YA KUEPUKA KUTONESHA MAJERAHA WAATHIRIKA UKATILI WA KINGONO

Na INNOCENT KANSHA- Mahakama, Dodoma.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo leo tarehe 04 Februari, 2025 amefungua mafunzo ya kuepuka kutonesha majeraha kwa waathirika wa ukatili wa kingono (Avoiding re-traumatization of victims and witnesses of sexual and gender-based violance) mafunzo hayo yanatolewa kwa Mahakimu Wakazi, Waendesha Mashtaka na Maafisa Ustawi wa Jamii.

Mafunzo hayo yanayofanyika katika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) jijini Dodoma yanaendeshwa na Chuo cha Uongozi wa Mahakama - Lushoto (IJA) kwa kushirikiana na Taasisi ya Kimataifa ya Irish Rule of Law International (IRLI) chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Ireland nchini Tanzania.

“Leo tumekutana hapa Maafisa Mahakama, Waendesha Mashtaka na Maafisa ustawi wa Jamii kujifunza, kujadili kwa umoja wetu na kuchangia uzoefu wetu wa namna ya kukabiliana na aina hii ya mashauri kwa uangalifu, ufanisi mkubwa na weledi wa hali ya juu,” amesisitiza Mhe. Dkt. Masabo.

Aidha, Mhe. Dkt. Masabo ameishukuru Irish Rule of Law International (IRLI) katika kufanikisha mafunzo hayo pamoja na juhudi zao za kudumisha utawala wa Sheria, bila kuwasahau IJA pamoja na Mahakama ya Tanzania kupitia Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma aliyebariki kufanyika kwa mafunzo hayo.

“Kazi yetu kubwa leo ni kuhakikisha tunatoka na mbinu wezeshi na rafiki za kuhakikisha waathirika wa unyanyasaji wa kijinsia na kingono wanahudumiwa kwa kuzingatia utu, nidhamu na heshima ili kuondoa na kuepuka kutonesha majeraha ya waathirika wa ukatili huo,” amesema Jaji Masabo.

Mhe. Dkt. Masabo ameongeza kuwa, watu wengine huwaita waathirika ama walionusurika kwenye vitendo vya unyanyasaji ila majina hayo yote hayajalishi bali ni jukumu lenu la msingi pale mtapokutana na waathirika hao mfanye nao kazi ili kuhakikisha wanahudumiwa kwa kuzingatia utu na heshima.

“Hii ina maanisha kwamba, kutumia lugha nzuri, nyepesi na ya huruma, kuwa wavumilivu pale waathirika hao wanaposhindwa kujielezea kwa ufasaha wawapo maeneo yenu ya kazi ili kutengeneza mazingira ya mahakamani kuwa salama kwake na kumtengenezea mazingira rafiki awapo mahakamani. Pia tunatakiwa kutambua kwamba mshitakiwa naye ana haki za msingi ambazo zinatakiwa kuheshimiwa ili haki iweze kutendeka bila upendeleo. Kwa muktadha huo hii ni kazi ngumu kwa pande zote mbili zinazopigania haki. Haki ya mwathirika kwa upande mmoja na na haki ya mtuhumiwa kwa upande mwingine ili kuhakikisha na kuona haki imetendeka bila upendeleo,” amehimiza Jaji Mfawidhi.

Vilevile, Jaji Mfawidhi huyo amesema, ameipitia ratiba ya mafunzo na mada zitakazo tolewa na wakufunzi na kujiridhisha kuwa, watawapitisha katika njia za kuepuka kutonesha majeraha ya waathirika wa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia na kingono na kwa kupitia mada hizo na nyingine zitasaidia kujadili mbinu zinazotumika kwa sasa na kuainisha maeneo ya kuboresha mbinu hizo.

Katika hotuba yake, Mhe. Dkt. Masabo amewaasa washiriki hao kuzingatia yale yote watakayofundishwa kwenye mafunzo hayo, kushiriki kikamilifu na kuuliza maswali inapobidi na kuchangia uzoefu ili kujenga uelewa mzuri na wa pamoja kwa kuhakikisha waathirika wa ukatili wa kingono wanakuwa na mazingira rafiki kipindi wanatoa ushahidi wao Mahakamani.

“Ujuzi na maarifa tutakayojengewa kupitia mafunzo haya visihishie hapa na kwetu peke yetu mathalani nimebaini katika mafunzo haya hawapo Mawakili wa kujitegemea (Practising Advocates) kwenye kundi hili, ni rai yangu mkawashirikishe maarifa haya wenzenu mnaofanya nao kazi, elimu mliyoipata hapa pindi mtakapo rejea makazini, mfano binu za kuuliza maswali kwa waathirika wa vitendo vya ukatili wa kingono ni jambo la msingi sana kwa Mawakili wanaowawakilisha watu wenye mashauri ya aina hii,” ameongeza Jaji Masabo

Mhe. Dkt. Masabo ameongeza kuwa, Mahakama ya Tanzania pamoja na IJA wataandaa mpango wa kufanya tathmini ya utekelezaji kuona kama kweli mafunzo hayo yamewasaidia washiriki kupiga hatua katika kushughulikia na uendeshaji wa mashauri hayo yanapofika mahakamani na kutoa matokeo chanya.

Mhe. Dkt. Masabo akahitimisha kwa kuwataka washiriki wa mafunzo hayo kufanya kazi kwa ushirikiano ili kufanya mfumo wa utoaji haki kuwa rafiki na wenye ufanisi mkubwa katika kuendesha mashauri ya ukatili wa kijinsia na unyanyasaji wa kingono kwa kuzingatia maslahi mapama ya waathirika wa vitendo hivyo na pia bila kuathiri haki za watuhumiwa wa vitendo hivyo.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo leo tarehe 04 Februari, 2025 amefungua mafunzo ya kuepuka kutonesha majeraha kwa waathirika wa ukatili wa kingono (Avoiding re-traumatization of victims and witnesses of sexual and gender-based violance) mafunzo hayo yanatolewa kwa Mahakimu Wakazi, Waendesha Mashtaka na Maafisa Ustawi wa Jamii.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo leo tarehe 04 Februari, 2025 amefungua mafunzo ya kuepuka kutonesha majeraha kwa waathirika wa ukatili wa kingono (Avoiding re-traumatization of victims and witnesses of sexual and gender-based violance) mafunzo hayo yanatolewa kwa Mahakimu Wakazi, Waendesha Mashtaka na Maafisa Ustawi wa Jamii.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo (katikati) akiwa meza Kuu wakati wa hafla fupi ya kufungua mafunzo hayo, wengine ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Tabora Mhe. Dkt. Zainabu Mango (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji kutoka Irish Rule of Law International Bi. Maria Mccloskey.


Mwezeshaji wa mafunzo hayo na Mahakimu Wakazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya ya Momba Mhe. Raymond Kaswaga akifafanua jambo.

 

Timu ya Irish Rule of Law International (IRLI) ikiongozwa na Bw. Sean Mchale na Mkurugezi wa masuala ya dawati la unyanyasaji na Ukatili wa Kijinsia Bi. Oliver Kinabo.


Sekretarieti ya Mafunzo hayo ikiongozwa na Afisa Utumishi Mahakama ya Wilaya Dodoma Bi Arapha Lusheke (kushoto) na watumishi wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto IJA Bw. Gidion Songa 

 

Mkurugenzi Mtendaji kutoka Irish Rule of Law International Bi. Maria Mccloskey akifafanua jambo wakati  wa hafla ya kufungua mafunzo ya ukatili wa kijinsia na ukatili wa kingono .




Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Timu ya Irish Rule of Law International (IRLI) ikiongozwa na Bw. Sean Mchale na Mkurugezi wa masuala ya dawati la unyanyasaji na Ukatili wa Kijinsia Bi. Oliver Kinabo.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Maafisa Mahakama wanaoshiriki mafunzo ya kuepuka kutonesha majeraha kwa waathirika wa ukatili wa kingono. Wengine ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Tabora Mhe. Dkt. Zainabu Mango (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji kutoka Irish Rule of Law International Bi. Maria Mccloskey.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Waendesha Mashtaka wanaoshiriki mafunzo ya kuepuka kutonesha majeraha kwa waathirika wa ukatili wa kingono. Wengine ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Tabora Mhe. Dkt. Zainabu Mango (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji kutoka Irish Rule of Law International Bi. Maria Mccloskey.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Maafisa Ustawi wa Jamii wanaoshiriki mafunzo ya kuepuka kutonesha majeraha kwa waathirika wa ukatili wa kingono. Wengine ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Tabora Mhe. Dkt. Zainabu Mango (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji kutoka Irish Rule of Law International Bi. Maria Mccloskey.

Mkufunzi wa mafunzo hayo na Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Victoria Nongwa akifafanua jambo kwa washiriki wa mafunzo hayo.

 
Sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo wakiwa kwenye ukumbi wa mafunzo.


Mkufunzi wa mafunzo hayo na Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Victoria Nongwa akifurahia jambo na sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo.





(Picha na Innocent Kansha -Mahakama)

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni