Na Fredrick Mahava - Mahakama, Sumbawanga.
Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Dkt. Deo John Nangela
ameshiriki maadhimisho ya sherehe ya siku ya sheria nchini Mahakama Kuu ya
Tanzania, Kanda ya Sumbawanga na kuzindua ripoti ya utendaji kazi wa mwaka 2024
zoezi ambalo litakuwa endelevu kila mwishoni mwa mwaka la utaratibu wa kutoa
ripoti ya utendaji kazi wa Kanda hiyo.
Ripoti hiyo chenye sura sita imeangazia mambo
mbalimbali ya kiutendaji katika Kanda hiyo, ikiwemo historia ya Mahakama Kuu ya
Tanzania, Kanda ya Sumbawanga tangu ilipoanzishwa mwaka 2005 kikionyesha picha
za Majaji Wafawidhi waliyowahi kuhudumia Kanda hiyo katika vipindi tofauti hadi
mwaka 2023.
Aidha, sura nyingine zimezungumzia hali ya Watumishi,
Takwimu za Mashauri, Majengo na viwanga vya Mahakama, matumizi ya mifumo ya
kielektroniki, vyombo vya moto vya usafiri pamoja na bajeti inayotumika
kuendesha shughuli za Mahakama Kanda ya Sumbawanga.
Akifafanu yaliyomo kwenye ripoti hiyo, Mtendaji wa
Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga Bw. Machumu Elias Essaba alisema, kitabu hicho
ni nyenzo itakayopima utendaji wa Mahakama zote za Kanda ya Sumbawanga mwaka
2025 ikilinganishwa na kazi zilizofanyika mwaka 2024.
Mahakama zote za Sumbawanga zimemaliza mwaka 2024
zikiwa na wastani wa kumaliza mashauri kadri yalivyosajiwa kwa asilimia 103%.
Aidha wastani wa kumaliza mashauri ya siku nyingi (disposal rate) ilikuwa asilimia
82%. Mtendaji huyo ameongeza kuwa, Kulikuwa na mashauri mawili peke yake
yaliyokuwa kwenye mlundikano wa mashauri. Viwango hivyo vitatakiwa kuongezeka
na siyo kurudi tena nyuma.
Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Dkt. Nangela akiwaonesha kitabu chenye ripoti ya utendaji kazi wa Kanda ya Sumbawanga Waheshimiwa Majaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga, Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa Mhe. Nyakia Ally Chirukile pamoja na hadhara iliyokusanyika kwa ajili ya maadhimisho ya siku ya sheria.
Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Dkt. Deo Nangela akikata utepe na kukifungua kitabu chenye ripoti ya Utendaji kazi Kanda ya Sumbawanga.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni