Alhamisi, 6 Februari 2025

JAJI KIHWELO ATETA NA WASHIRIKI WA MAFUNZO

Na Arapha Rusheke, Mahakama Dodoma

Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) Mhe. Dkt. Paul F. Kihwelo amekutana na kuongea na washiriki wa mafunzo ya kuepuka kutonesha majeraha kwa waathirika wa ukatili wa kingono (Avoiding re-traumatization of victims and witnesses of sexual and gender-based violance) yanatolewa kwa Mahakimu Wakazi, Waendesha Mashtaka na Maafisa Ustawi wa Jamii.

Akizungumza na washiriki hao wanaoendelea na mafunzo hayo jana tarehe 5 Februari, 2025 ikiwa ni siku ya pili ya mwendelezo wa mafunzo hayo, yanayoendelea katika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) jijini Dodoma yakiendeshwa na Chuo cha Uongozi wa Mahakama-Lushoto (IJA) kwa kushirikiana na Taasisi ya Kimataifa ya Irish Rule of Law International (IRLI) chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Ireland nchini Tanzania.

“Niwapongeze sana kwa kuchaguliwa na taasisi zenu ambazo zinashiriki mafunzo haya tunapenda nyie mpate kile ambacho kimeandaliwa na wawezeshaji wetu, lakini upande mwingine tunapenda pia wawezeshaji nao ambao wamewakuta umu ndani wakute tumewachagulia washiriki sahihi, hii programu tunafanya na watu wa Irish Rule of Law International, tunapofanya mafunzo ambayo yanakuwa na wadau wengi kuna vitu vingi tunavipata kama ambavyo mnafahamu kesi Mahakamani hatufanyi peke yetu,” amesema Mhe. Dkt.Kihwelo.

Mhe. Dkt. Kihwelo aliongeza kuwa, mafunzo kwa namna nyingine yanabadilisha watu na kuwafanya waongeze umakini kama mnavyofahamu haiwezi kuwaleta watu wote kwa wakati mmoja, hivyo ninyi mliopo hapa mwende mkawape wenzenu ujuzi na maarifa mliyoyapata kwenye mafunzo haya.

“kuna kitu kimoja ambacho nilisema nikiseme kwa sababu ndicho tunachokitegemea mkitoka hapa, mafunzo haya mlioyapata mkayafanyie kazi  hilo ndiyo lengo kubwa zaidi, na pia tunategemea sana kupata matunda mazuri baada ya kutoka katika mafunzo haya. Niwapongeze kwa fursa hii na niwashukuru sana na kuwatakia kila la kheri, ninawashauri mkirudi katika vituo vyenu vya kazi jitahidini mlichokipata hapa muwafundishe na wenzenu,” amesema Mhe. Dkt. Kihwelo.

Mhe. Dkt. Kihwelo amehitimisha kwa kuwataka washiriki wa mafunzo hayo kufanya kazi kwa ushirikiano ili kufanya kazi iwe rahisi na yenye ufanisi mkubwa.

Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) Mhe. Dkt.Paul F. Kihwelo (katikati) akiwa Meza Kuu wakati alipokuja kuongea na washiriki wa  mafunzo hayo, wengine ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Tabora Mhe. Dkt. Zainabu Mango (kushoto) na Mkufunzi wa mafunzo hayo na Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Victoria Nongwa (kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na washiriki ambao ni Mahakimu wakazi kutoka sehemu mbalimbali hapa Nchini.

Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) Mhe. Dkt.Paul F. Kihwelo (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Maafisa Ustawi wa Jamii wanaoshiriki mafunzo ya kuepuka kutonesha majeraha kwa waathirika wa ukatili wa kingono. Wengine ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Tabora Mhe. Dkt. Zainabu Mango (kushoto) na na Mkufunzi wa mafunzo hayo na Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Victoria Nongwa.

Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) Mhe. Dkt.Paul F. Kihwelo (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Waendesha Mashtaka wanaoshiriki mafunzo ya kuepuka kutonesha majeraha kwa waathirika wa ukatili wa kingono. Wengine ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Tabora Mhe. Dkt. Zainabu Mango (kushoto) na na Mkufunzi wa mafunzo hayo na Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Victoria Nongwa.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni