Na. Daniel Sichula-Mahakma Mbeya
Jaji
Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga
aliwaongoza Watumishi wa Mahakama hiyo kutembelea Gereza la Ruanda lililopo
Jijini Mbeya hivi karibuni kupeleka misaada mablimbali ya kibinadamu katika
Gereza hilo.
“Watumishi
wa Mahakama na wadau wengine wa sheria tunawajali, tunayo furaha kufika hapa kuwapatia
elimu pamoja na misaada mbalimbali ya kibinadamu katika Maadhimisho haya ya wiki
na siku ya Sheria Nchini,” alisema Jaji Tiganga.
Vilevile,
Mhe. Tiganga alielezea kuwa, tukio hilo la kupeleka misaada kwenye Gereza ni
kuonyesha upendo kwa Wafungwa waliopo katika Gereza hilo na kuendelea kwa
kusema kuwa watakuwa wakifanya hivyo mara kwa mara kwa wafungwa hao na wa
Magereza mengine yaliyopo katika Mkoa huo wa Mbeya.
Naye,
Kamishina Msaidizi wa Gereza hilo Bw. Mwitiki Kupya kwa niaba ya Uongozi wa
Gereza hilo aliwashukuru Mahakama Kanda ya Mbeya pamoja na wadau wote wa sheria kwa
kujitoa kwao kwa hali na mali kuwasaidia wafungwa pamoja na mahabusu waliopo
gerezani hapo.
“Misaada
hii ni ishara tosha kuwa Mahakama ya Tanzania walivyo na upendo kwa Magereza
hapa Nchini ni mategemeo yangu mtaendelea kutupa misaada hii kwasababu ina
mssada mkubwa kwa wafungwa,” alisema Kamishina Msaidizi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni