Jumanne, 18 Februari 2025

MAAFISA MAHAKAMA LINDI WAFUNDWA MATUMIZI YA e-JOPRS

·  Wafundishwa juu ya Mfumo wa Kidigitali wa Tathimini na Mapitio ya Utendaji wa Maafisa Mahakama (ELECTRONIC JUDICIAL OFFICERS OPEN PERFORMANCE REVIEW AND APPRAISAL SYSTEM–e-JOPRAS).

·      Waaswa kuendana na kasi ya Mahakama ya Tanzania juu ya Matumizi ya  Mifumo ya KITEHAMA.

·  Wasisitizwa kuishi kauli mbiu ya Mahakama ya Tanzania ambayo ni Uadilifu, Ueledi na Uwajibikaji.

Na HILARY LORRY – Mahakama, Lindi

Maafisa Mahakama Mkoa wa Lindi wamepata mafunzo ya matumizi ya Mfumo kidigitali wa tathmini na mapitio ya utendaji wa maafisa Mahakama mahususi kwa Majaji na Mahakimu (eJOPRAS).

Mafunzo hayo, yamefanyika hivi karibuni katika ukumbi wa wazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi yakiratibiwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe. Consolata Peter Singano pamoja na Afisa Tehama wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Bw. Furaha Khatibu.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mafunzo hayo Mhe. Singano alisema Mahakama ya Tanzania imeona umuhimu wa kuanzisha mfumo huu  kwa lengo la  kuhakikisha  uwajibikaji, uwazi na maendeleo endelevu ya taaluma kwa kuweka malengo yanayoweza kupimwa, kufuatiliwa na kupata mrejesho.

Mhe. Singano aliwakumbusha Mahakimu juu ya hatua kubwa iliyopigwa na Mahakama ya Tanzania katika Matumizi ya mifumo ya TEHAMA na kuwataka maafisa hao kuendana na kasi hiyo.

Aidha, aliwasisitiza Mahakimu kuzingatia maadili ya kazi zao ili waweze kutekeleza majukumu yao ya utoaji haki kwa ufanisi unaotakiwa bila ya kufanya upendeleo wa aina yoyote kwa wateja wao.

“Nawasihi kila mmoja wetu afanye kazi yake kwa uamnifu mkubwa bila ya upendeleo kwa upande wowote, huku tukitambua kuwa kazi hii tunayofanya si kazi yetu bali ni kazi ya Mungu na tufanye kwa uaminifu tukiongozwa na kauli mbiu ya Mahakama ya Tanzania ya Uadilifu, Ueledi na Uwajibikaji. Tukiweza kuishi kauli mbiu hiyo ninayo hakika kwamba wananchi na jamii kwa ujumla itarithishwa na maamuzi yetu na kuzidi kurejesha imani ya wananchi juu Mahakama Tanzania na jukumu lake mama la utoaji haki,” alisema Mhe. Singano.

 Afisa Tehama Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Bw. Furaha Khatibu pamoja na Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe.Singano kwa nyakati tofauti tofauti waliwasisitiza Mahakimu walioshiriki Mafunzo hayo kuzingatia zoezi la uhuishaji wa taarifa katika mifumo ya kuratibu mashauri (e-CMS) pamoja na mfumo wa kuratibu mashauri Mahakama za mwanzo (Primary Court App) kwani mifumo hiyo inafanyakazi sambamba na mfumo wa Tathimini na Mapitio ya Utendaji wa Maafisa wa Mahakama (e-JOPRAS).

Vilevile, Baada ya Mafunzo hayo Maafisa Mahakama walipata wasaa wakutembelea na kuona maendeleo ya ujenzi wa Kituo Kidogo Jumuishi Lindi (MINI IJC LINDI) unaoendelea chini ya kampuni ya RIVZI ENGENIARING COMPANY LIMITED.

Mafunzo yalihudhuriwa na Hakimu Mkazi Mkuu Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe. Consolata Peter Singano, Hakimu Mkazi Mwandamizi Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe. Delphina Kimath na Mahakimu Wakazi wa Wilaya tano (5) zinazopatikana katika Mkoa wa Lindi pamoja na Mahakimu wa Mahakama zote za Mwanzo na Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Bi. Quip Godfrey Mbeyela.

Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe.Consolata Peter Singano (aliyevaa suti ya dark blue) akiwa kwenye picha ya pamoja na MaafisaV Mahakama walioshiriki Mafunzo ya Mfumo wa Tathimini na Mapitio ya Utendaji wa Maafisa wa Mahakama (ELECTRONIC JUDICIAL OFFICERS OPEN PERFORMANCE REVIEW AND APPRAISAL SYSTEM –eJOPRAS).

Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe.Consolata Peter Singano (aliyevaa suti ya dark blue) akitoa neno la ufunguzi kwa maafisa walioshiriki Mafunzo ya Mfumo wa Tathimini na Mapitio ya Utendaji wa Maafisa wa Mahakama (ELECTRONIC JUDICIAL OFFICERS OPEN PERFORMANCE REVIEW AND APPRAISAL SYSTEM –eJOPRAS).

Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Bi. Quip Godfrey Mbeyela (aliyesimama) akitoa neno la ukaribisho kwa Maafisa Mahakama walioshiriki mafunzo hayo.

Afisa Tehama Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Bw. Furaha Khatibu (aliyesimama) akiwasilisha mada wakati wa mafunzo hayo.






Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe.Consolata Peter Singano (aliyevaa suti ya dark blue) akiwa kwenye picha ya pamoja na MaafisaV Mahakama walioshiriki Mafunzo ya Mfumo wa Tathimini na Mapitio ya Utendaji wa Maafisa wa Mahakama (ELECTRONIC JUDICIAL OFFICERS OPEN PERFORMANCE REVIEW AND APPRAISAL SYSTEM –eJOPRAS).

Washiriki wakifuatilia kwa makini mada zinazowasilishwa na Afisa Tehama.

Washiriki wakifuatilia kwa makini mada zinazowasilishwa na Afisa Tehama.


Afisa Tehama Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Bw. Furaha Khatibu (aliyesimama) akiwasilisha mada wakati wa mafunzo hayo.







Hakuna maoni:

Chapisha Maoni