Na DANIEL SICHULA – Mahakama, Mbeya
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga tarehe
12 Februari, 2025 ahitimisha mafunzo ya mfumo wa upimaji na kutathmini utendaji
kazi kwa Mahakimu wa Mahakama Mkoa wa Mbeya.
Katika
maboresho ya utendaji kazi kwa watumishi wa Mahakama, Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya
iliendesha mafunzo maalum kwa Mahakimu wa Mkoa wa Mbeya katika matumizi
mbalimbali ya Mifumo ya kielektroniki ikiwa ni jitihada za kuongeza ufanisi wa
utendaji kazi kwa watumishi hao.
Wataalam
wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHEMA) wa Mahakama Kuu Mbeya na
Songwe, Bw. Sadati Kalungwana na Bi. Rosemary Mwandambo, walitoa elimu ya
mifumo ya kielektroniki namna ya utumiaji wa mifumo kama eJOPRAS, eCMS na Data Hub
kwa Mahakimu na umuhimu wa mifumo hiyo katika utendaji wao wa kazi za kila
siku.
Aidha,
washiriki walipata kujua namna ya kutumia mfumo wa eJOPRAS katika majukumu yao
ya kila siku na namna ya kujaza taarifa zao kwani mfumo huo ni muhimu katika
kutathmini utendaji wao wa kazi na kupata mrejesho wa kile wanafanyia kazi kila
siku.
Umuhimu
wa mfumo eJOPRAS ulionekana pale Mahakimu walipojaribu kufanya kwa vitendo na
kuona ni namna gani mfumo huo utakua na msaada katika kazi zao za kila siku.
Mafunzo
hayo yaliwapa Mahakimu uelewa wa kina wa namna ya kutumia mfumo huo kwa
ufanisi, ikiwa ni pamoja na mbinu za kuhakikisha tathmini zao zinasaidia
kuimarisha huduma kwa Wananchi.
Na
katika Mfumo wa eCMS washiriki waliweza patiwa ujuzi zaidi kwani wamekuwa
wakiutumia mara kwa mara katika usajili wa mashauri, usikilizwaji wa mashauri
na kutolea maamuzi kwa wakati na kupunguza ucheleweshaji wa mashauri.
Na
pia, Mahakimu hao walishukuru uongozi wa Mahakama Kuu Mbeya kwa kuendesha
mafunzo ya mifumo ya kielectroniki, kwani imewakumbusha uwajibikaji katika majukumu
yao ya kila siku katika kuwahudumia wananchi kwa haki na kwa ufanisi.
Afisa TEHAMA Bw. Sadati Kalungwanasadati
akifafanua namna mfumo wa ejopras unavyofanyakazi.
Mahakimu
wakiwa kwenye mafunzo ya mifumo ya kieletroniki.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni