Na ARAPHA RUSHEKE-Mahakama Kuu, Dodoma
Mahakama
Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma imefanya hafla fupi ya kumuaga aliyekuwa Jaji wa Mahakama Kuu Dodoma, Mhe. Edwin Eliasi Kakolaki, ambaye amehamishiwa Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara
kuwa Jaji Mfawidhi.
Hafla
hiyo ilifanyika jana tarehe 20 Februari, 2025 katika Ukumbi wa Kituo Jumuishi
cha Utoaji Haki Dodoma na kuhudhuriwa na Majaji, Viongozi na Watumishi wengine.
Akizungumza
wakati wa hafla hiyo, Mhe. Kakolaki aliwashukuru Watumishi wa Mahakama Dodoma
kwa ushirikiano na upendo mkubwa waliompatia wakati akiwa katika Kanda hiyo.
Aliongeza
kwamba alikuwa na furaha ya kufanya kazi na timu imara na yenye ufanisi wa hali
ya juu ambao ulimwezesha kutekeleza majukumu yake bila kikwazo chochote.
"Nimefurahi
sana kufanya kazi na timu hii ya Mahakama Kuu Dodoma, ushirikiano wenu na
upendo mkubwa mlionionyesha umenisaidia kutekeleza majukumu yangu bila kikwazo
chochote…
“…kwa
kweli Dodoma ni eneo nililoishi kwa amani sana, ni eneo ambalo watu wana upendo,
ninawashukuru kila mmoja kwa nafasi yake kwa sababu mmekuwa mchango mkubwa
katika maisha yangu, nawapenda sana asanteni," alisema Mhe. Kakolaki.
Kwa
upande wake, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe.
Dkt. Juliana Masabo, kwa niaba ya Watumishi wote, alimpongeza
Jaji Kakolaki kwa kuaminiwa na kukasimiwa mamlaka ya kusimamia Kanda ya Mahakama
Mtwara.
“Hongera
sana, tunaungana na wewe kumshukuru Mungu kwa namna ambavyo amekulinda, amekutunza
na kwa mema yote ambayo amekutendea, lakini zaidi kwa namna ambavyo amekuona
kama unafaa na kutoa kibali ili uweze kusimamia Kanda ya Mtwara,” alisema.
Mhe.
Dkt. Masabo alitumia fursa hiyo kumshukuru Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahimu
Hamis Juma na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed
Siyani kwa imani waliyoionesha na kumteua Mhe. Kakolaki kuwa Jaji Mfawidhi katika
Mahakama Kanda ya Mtwara.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mtwara, Mhe. Edwin Eliasi Kakolaki akiwa katika uso wa bashasha mara baada ya kupokea moja ya zawadi kutoka kwa Watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma. Picha chini akipokea zawadi nyingine kutoka kwa Watumishi.
Baadhi ya Watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma wakiwa katika
picha ya pamoja wakati wa hafla hiyo.
Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dar es Salaam.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni