Na MAGRETH KINABO-Mahakama, Dodoma
Jumla ya Majaji sita wa Mahakama ya Rufani Tanzania leo tarehe 10 Februari, 2025 wameanza vikao vya kusikiliza mashauri 52 mbalimbali ya madai katika majopo ya makundi mawili kwenye jengo la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania lililopo jijini Dodoma.
Kwa mujibu wa Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Mhe. Omari Kingwele aliwataja Majaji waliopo katika jopo la kundi A kuwa ni Mhe. Dkt. Mary Caroline Levira.Majaji wengine ni Mhe.Zepharine Nyalugenda Galeba na Mhe. Mustapha Kambona Ismail.
Naibu Msajili huyo amesema Majaji hao wanatarajia kusikiliza mashauri 26, ambayo ni ya mlundikano yanayohusu masuala ya kodi na biashara.
Katika hatua nyingine Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Mhe. Charles Magesa amesema jopo lingine la kundi B la Majaji watatu, ambao ni Mhe. Rehema Kerefu, Mhe. Patricia Saleh Fikirini na Mhe. Benhajj Shabaan Masoud litasikiliza mashauri 26, ambayo ni kodi, biashara na ardhi.
Majaji hao wanatarajia kumaliza vikao hivyo vya kusikiliza mashauri hayo tarehe 28 Februari, 2025.
Baadhi ya Majaji sita wa Mahakama ya Rufani Tanzania waliowasili jijini Dodoma kwa ajili kuanza vikao vya kusikiliza mashauri ya madai katika jengo la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania lililopo jijini Dodoma. wakiwemo wawili wapya walioripoti kwenye kituo chao cha kwanza cha kazi wakiwa katika pichaya pamoja.
Baadhi ya Mawakili wakijiandaa kwa ajili ya vikao vya mashauri hayo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni