Na Fredrick Mahava – Mahakama, Sumbawanga
Mahakimu
Kanda ya Sumbawanga wamepata mafunzo ya mfumo wa kidigitali wa tathimini na
mapitio ya utendaji (e-JOPRAS) ikiwa ni jitihada za kuongeza utendaji kazi.
Mafunzo
hayo yalifunguliwa na Kaimu Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawangu Mhe.
Dkt. Thadeo Mwenempazi tarehe 21 Februari, 2025 ambayo yalifanyika katika
Ukumbi wa Mahakama Kuu.
Mafunzo
hayo yaliendeshwa na Afisa TEHAMA wa Mahakama Kuu Sumbawanga Bw. Mayanga Someke
aliyewajengea uwezo wa namna ya kutumia
mfumo wa e-JOPRAS katika majukumu yao ya
kila siku na namna ya kujaza taarifa zao kwenye mfumo huo kwa ufanisi. Mahakimu
hao walipata uelewa wa namna mfumo huo unavyofanya kazi kwa vitendo.
Aidha,
kabla ya mafunzo hayo, yalitanguliwa na kikao cha watumishi wa Mahakama Kuu, Kanda
ya Sumbawanga na Katavi ambao walipewa mrejesho wa mambo mbalimbali ambayo
yalitokana na kikao cha mapitio ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2024/2025 kwa
kipindi cha nusu mwaka na maandalizi ya bajeti ya mwaka 2025/2026
kilichofanyika Dodoma.
Akizungumza
wakati wa kikao hicho Mtendaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga Bw. Machumu
Essaba alitoa taarifa ya
bajeti ya mwaka fedha 2025/2026 kwa Mahakama zilizopo mkoa wa Rukwa na pia alitoa mrejesho
wa maelekezo kutoka kwa Mtendaji Mkuu
kuhusu utekelezaji.
Vilevile,
Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga Mhe. Joseph Luambano alitoa
msisitizo juu ya matumizi ya TEHAMA katika usikilizaji wa mashauri na
kuzingatia nyaraka mbalimbali zilizotelewa na Jaji Mkuu, Jaji Kiongozi na
Msajili Mkuu. Pia aliwaomba watumishi kuendelea kusimamia mikakati iliyowekwa
ambayo ilisaidia kupunguza mlundikano wa mashauri.
Naye,
Kaimu Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga Mhe. Dkt. Thadeo
Mwenempazi pamoja Jaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga Mhe. Abubakar
Mrisha, Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Mhe. Joseph Luambano na
Mtendaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga Bw. Machumu Essaba waliungana na
Mahakimu kupata mafunzo hayo.
Kaimu Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga Mhe. Dkt. Thadeo Mwenempazi akifungua mafunzo ya e-JOPRAS kwa Mahakimu katika Ukumbi wa Mahakama Kuu Sumbawanga
Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Mhe. Joseph Luambano akisisitiza jambo kwa Mahakimu hao wakati wa mafunzo.
Mtendaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga Bw. Machumu Essaba akitoa mrejesho wa kikao cha Bajeti kilichofanyika jijini Dodoma hivi karibuni
Majaji na Mahakaimu wakifuatilia kwa makini Mafunzo ya Mfumo wa e-JOPRAS
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni