Na Christopher Msagati – Mahakama, Manyara
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Manyara Mhe. John Rugalema
Kahyoza, amewaongoza watumishi wa Mahakama Kanda hiyo, kufanya ziara ya utalii
iliyofanyika mnamo tarehe 22 Februari, 2025 katika Hifadhi ya Bonde la
Ngorongoro (Ngorongroro Crater) mkoani Arusha.
Akizungumza
na watumishi kwa nyakati tofauti wakati wa maandalizi na hitimisho la ziara
hiyo, Mhe. Kahyoza alieleleza lengo la ziara hiyo ni kutambua maeneo mapya
ambayo watumishi wengi hawajawahi kuyafikia, kupata furaha na kuimarisha afya
ya akili.
“Muda
mrefu tunakaa ofisini tukiwa tunashughulika na majukumu ya usikilizwaji wa
mashauri bila kupata fursa ya kufahamu masuala mengine mengi ambayo tunapaswa
kuyafahamu. Hili jambo linaweza kupunguza ufanisi wa utendaji kazi kama
tunakosa muda wa kuwaza masuala mengine nje ya kazi, ziara hii ya Ngorongoro
ituwezeshe kuwa na mtazamo mpya lakini pia kuyafahamu maeneo ambayo
yanatuzunguka,” alisema Mhe. Kahyoza.
Kwa
upande wake, Jaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Manyara Mhe. Devotha Kamuzora
aliwapongeza watumishi wote waliofanikiwa kushiriki ziara hiyo na kuwashauri
watumishi kuendelea kushirikiana katika masuala kama hayo yanapojitokeza kwa
kuwa pia yanaongeza upeo wa ufahamu ambao unaimarisha utendaji kazi.
“Nawapongeza
watumishi wote (Watalii wenzangu) waliofanikiwa kusafiri kwa ajili ya utalii na
nawashauri siku nyingine ziara kama hii ikitokea tuungane sote kwa pamoja kwa
kuwa tutakuwa tumeongeza kitu kikubwa sana katika upeo na ufahamu wetu na
kuboresha ufanisi wa kazi pia,” alisema Mhe. Kamuzora.
Vilevile,
Mhe. Kahyoza aliwashukuru watumishi wa Mahakama ya Wilaya ya Karatu kwa
kushirikiana nao bega kwa bega katika maandalizi ya safari hiyo ya kuelekea
Ngorongoro.
Watumishi
66 wa Kada tofauti kutoka Mahakama za ngazi mbalimbali wakiwemo Mahakimu
Wakazi wafawidhi wa Wilaya zilizopo katika Kanda ya Manyara, Mahakimu wengine
na Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Manyara walishiriki ziara hiyo ikiwa ni
muendelezo wa kuendelea kutambua vivutio vya asili vilivyo ndani na nje ya Mkoa
wa Manyara pamoja na kuwafanya watumishi kuendelea kuishi kwa umoja na kwa
ushirikiano.
Watumishi
wa Mahakama Kuu Kanda ya Manyara wakiwa katika picha ya Pamoja katika ziara ya
Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Manyara Mhe. John Kahyoza (wa kwanza kulia) akiwa katika picha ya Pamoja na baadhi ya watumishi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Manyara katika ziara ya Hifadhi ya Taifa Ngorongoro.
Tembo
akionekana katika Eneo la Ngorongoro Crater wakati wa ziara ya Hifadhi ya Taifa
Ngorongoro iliyofanywa na watumishi wa Mahakama Kuu Kanda ya Manyara.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni