Na Fredrick Mahava- Mahakama, Sumbawanga
Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Augustine Mwarija
ameongoza kikao cha tathmini ya jopo la Mahakama ya Rufani kilichoketi Mahakama
Kuu, Kanda ya Sumbawanga. Aidha kwa mujibu wa Kalenda ya Mahakama ya Rufani kikao
hicho ni cha kwanza kwa mwaka 2025 kilichoanza tarehe 10 Machi, 2025 na
kinatarajiwa kuhitimishwa leo tarehe 28 Machi, 2025.
Katika kikao hicho jumla
ya mashauri 28 yalipangwa kusikilizwa na mashauri yote yamefanikiwa kusikilizwa
ikipelekea ufanisi wa asilimia 100 ya mashauri yote yaliyopangwa.
Aidha, katika mashauri
hayo 28, Mashauri 17 yameshatolewa maamuzi, Mashauri 11 bado yanasubiria kutolewa maamuzi na hakuna shauri
lililohairishwa.
Vilevile, Mhe. Mwarija ambaye alikuwa Mwenyekiti wa jopo la
Majaji wa Mahakama ya Rufani waliosikiliza mashauri hayo kwa kushirikiana na
Majaji wengine wa Mahakama hiyo ambao ni Mhe. Lilian Mashaka na Mhe. Dkt. Eliezer
Mbuki Feleshi kwa pamoja walisikiliza mashauri ya Jinai 24 na Mashauri ya Madai
2 na maombi ya madai 2.
Pia tumefanikiwa kusajili mashauri yote yalipangwa katika
mfumo (eCMS) na mashauri yaliyomalizika tumeweza kuingiza taarifa hizo kwenye mfumo.
Akieleza sababu moja wapo ya mafanikio hayo, Mhe. Mwarija ni
ushirikiano walioupata kutoka kwa wadau wote wa mahakama kama vile Jeshi la
Magereza mkoa wa Rukwa kwa kuwawaisha
wafungwa mapema Mahakamani na Mawakili kwa ujumla kufika mapema kumewarahisishia
wao kufanya kazi kwa urahisi na kumaliza mashauri mapema
Wakati huohuo, Jopo la Majaji wa Mahakama ya Rufani ya
Tanzania walioketi Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga walieleza changamoto moja
kubwa ya mawakili kushindwa kusajili orodha ya mashauri kuegemewa (list of
Authority) kwa wakati na hivyo kuomba kutumia mashauri hayo wakati wa
usikilizwaji wa mashauri husika mahakamani.
Naye, Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani, Mhe.
Judith.J.Kamala aliwashukuru, Jeshi la
Mageleza, Polisi, Mawakili wa Serikali, Mawakili wa kujitegemea, Ofisi ya
Mwendesha Mashtaka wa Serikali kwa ushirikiano waliouonesha na pia alilishukuru
Jopo hilo la Majaji wa Mahakama ya Rufani kwa kuendesha mashauri ya Rufaa hayo
kwa haki na kuwasaidia maafisa walioshiriki katika kikao hicho kujifunza mambo
mengi katika utekelezaji wa sheria na utoaji haki kwa wananchi kwa wakati.
Vilevile, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda
ya Sumbawanga Mhe. Fredrick Manyanda, Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda
ya Sumbawanga Mhe. Abubakar Mrisha, Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Kanda ya
Sumbawanga Mhe. Joseph Luambano, Mtendaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga
Bw. Machumu Essaba na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa
Rukwa Mhe. Kisasila Saguda waliungana na wadau wengine wa haki jinai kushiriki
kikao hicho cha tathmini ya kikao cha Mahakama ya Rufani (Session)
kilichofanyika katika Kanda ya Sumbawanga.
Jaji
wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Augustine Mwarija akiongoza kikao cha
tathmini ya Kikao (Session) cha Mahakama ya Rufani kilichofanyika Kanda ya
Sumbawanga.
Naibu
Msajili wa Mahakama ya Rufani Mhe. Judith J.Kamala akizungumza wakati wa kikao
cha tathmini ya
kikao (Session) cha Mahakama ya Rufani kilichofanyika Kanda ya Sumbawanga.
Majaji
wa Mahakama ya Rufani Mhe. Lilian. L. Mashaka na Mhe. Dkt. Eliezer.M.Fereshi
wakifuatilia kwa ukaribu yanajiri kwenye kikao cha tathmini ya Kikao (Session) cha Mahakama ya
Rufani kilichofanyika Kanda ya Sumbawanga.
Wadau mbalimbali wa Haki Jinai
wakisikiliza kwa makini wakati wa kikao cha tathmini
ya Kikao
(Session) cha Mahakama ya Rufani kilichofanyika Kanda ya Sumbawanga.
(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni