Na Iman Mzumbwe – Mahakama, Songwe
Katika
kusherekea siku ya Kimataifa ya Majaji na Mahakimu Wanawake ambayo uadhimishwa
tarehe 10 Machi kila mwaka. Mahakimu Wanawake Wilaya ya Momba Mkoa wa Songwe
wamefanikiwa kutoa elimu ya Sheria katika Shule Sekondari ya Tunduma Town Council
inayohusu makosa ya kimtandao yenye kauli mbiu isemayo; ‘Haki katika zama za kidigitali
Majaji na Mahakimu Wanawake katika kushughulikia makosa ya kimtandao’
Mahakimu
hao, walitoa mada zilizoandaliwa na Chama cha Majaji na Mahakimu wanawake Tanzania
(TAWJA) zenye lengo la kuelimisha jamii juu ya Haki za msingi katika zama za
kidigitali na kufafanua mchango wa Majaji na Mahakimu Wanawake katika kushughulikia
makosa ya unyanyasaji wa ki-mitandao ya jamii.
Aidha,
Hakimu Mkazi Mwandamizi Mahakama Wilaya Momba Mhe. Tagha Emmanuel Komba alitoa
rai kwa wanafunzi wa shule hiyo ya sekondari kuto jihusisha na unyanyasaji wa
kimtandao kwani kufanya hivyo kunaweza kusababisha kushindwa kufikia malengo
yao ya msingi. Vilevile aliwaeleza
wanafunzi hao kuwa wasisite kutoa taarifa pindi wanapoona vitendo hivyo vya
unyanyasaji ili kusaidia kupunguza uovu huo katika jamii.
Naye,
Hakimu Mkazi Mkuu Mahakama ya Wilaya Momba Mhe. Magreth Moses Kannonyele
aliwasisitiza wanafunzi hao kuwa, watumie elimu hiyo kuielimisha jamii inayowazunguka
juu ya unyanyasaji wa kidigitali, kwani kwa kufanya hivyo itasaidia watu wengi
kutambua aina ya makosa hayo kwani yakibainika huzaa kosa la kijinai linaloweza
kupelekea kifungo au faini wakati mwingine vyote viwili kwa pamoja.
Kwa
upande wake, Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Tunduma Mhe. Demetria Simon alisema
kuna watu wanafanya unyanyasaji wa kimtandao bila kujua ni kosa kisheria ndiyo
maana ya kutoa elimu kwenu ili iwe chachu ya kuwaelimisha watu wengine kutambua
umuhimu wa kutotenda makosa ya aina hiyo.
Mahakimu
hao wanawake walioshiriki katika zoezi la utoaji elimu walikuwa Hakimu Mkazi
Mwandamizi Mahakama Wilaya Momba Mhe. Tagha Emmanuel Komba, Hakimu Mkazi Mkuu
Mahakama ya Wilaya Momba Mhe. Magreth Moses Kannonyele pamoja na Hakimu Mkazi
Mahakama ya Mwanzo Tunduma Mhe. Demetria Simon.
Hakimu Mkazi Mwandamizi Mahakama ya Wilaya Momba Mhe. Tagha Emmanuel Komba (mwenye suti ya bluu) akifafanua jambo wakati wa mafunzo hayo.
Hakimu Mkazi Mkuu Mahakama ya Wilaya Momba Mhe.
Magreth Moses Kannonyele (mwenye suti nyeusi) akielizea
juu ya unyanyasaji wa kimtandao unavyoathiri watoto katika jamii.
(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni