Alhamisi, 20 Machi 2025

WATUMISHI LINDI WAKUTANA KWENYE IFTAR YA PAMOJA

Na Hilari Herman - Mahakama, Lindi

Watumishi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi hivi karibuni walijumuika pamoja na Maafisa Mahakama na Maafisa wa Kada mbalimbali kupata iftar ya pamoja ikiwa ni sehemu ya kukutana, kufurahi pamoja na kubadilishana mawazo ili kudumisha ushirikiano baina yao.

Katika hafla hiyo iliyowakutanisha watumishi wa kada mbalimbali wa Mahakama hiyo, ilihudhuriwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe. Consolata Singano.

Akitoa neno wakati wa iftar hiyo kwa watumishi wa Mahakama waliofika katika hafla hiyo Mhe. Singano aliwasihi watumishi hao kuendelea kujirudisha kwa Mwenyezi Mungu kwa kufanya matendo yanayompendeza Mwenyezi Mungu hususani katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhan na Kwaresma.

Akinukuu maandiko mbalimbali kutoka katika vitabu vitakatifu, Mhe. Singano aliwakumbusha watumishi hao kuishi kwa kufuata misingi ya Imani zao, kupendana, kujaliana na kufanya kazi kwa pamoja na kushirikiana ili kuleta tija katika maeneo yao ya kazi.

“Kama tulivyokutana hapa kwenye iftar ya pamoja, basi ushirikiano huu uendelee katika maeneo yetu ya kazi kwa kufanya kazi kwa ushirikiano mkubwa,” alisisitiza Mhe. Singano.

Naye, Msaidizi wa kumbukumbu Mwandamizi wa Mahakama hiyo Bw. Suleiman Chikumba kwa niaba ya watumishi wote alitoa shukrani kwa Uongozi wa Mahakama hiyo kwa kuwakutanisha pamoja watumishi wa ngazi na kada mbalimbali katika “iftar ya pamoja” na kuuomba Uongozi wa Mahakama hiyo kulifanya tukio hilo kuwa ni endelevu kwani linaongeza ushirikiano baina ya watumishi.

Iftar hiyo iliitimishwa kwa dua nzito iliyosomwa na Afisa Ugavi Msaidizi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Ustaadh Abeid Omar.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe. Consolata Singano alieketi kwenye kiti akiwa na watumishi Wanawake wa Mahakama ya Lindi mara baada ya kupata iftar.

Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe. Consolata Peter Singano akitoa neno baada ya Iftar

Afisa Utumishi Mwandamizi wa Mahakama ya Hakimu Mazi Lindi Bw. Stephano Morey (kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe. Consolata Singano mara baada ya kupata iftar.

Afisa Ugavi Msaidizi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Ustaadh Abeid Omar akisoma dua mara baada ya watumishi kupata iftar.

Msaidizi wa kumbukumbu Mwandamizi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Bw. Suleiman Chikumba akitoa neno la shukrani mara baada ya iftar.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe. Consolata Singano alieketi kwenye kiti akiwa na watumishi wa Mahakama hiyo mara baada ya kupata iftar.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Mhe. Consolata Singano (kulia) akipata iftar pamoja na watumishi wengine wa Mahakama hiyo.

Afisa Utumishi Mwandamizi Mahakama ya Hakimu Mkazi Lindi Bw. Stephano Morey (kwanza kushoto) akishiriki iftar na watumishi wa Mahakama hiyo.

(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni