Na INNOCENT KANSHA - Mahakama
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Tabora, Mhe. Dkt. Adam Mambi
amesema kusipokuwa na msingi imara na mathubuti ya kiulinzi wa taarifa (Data
Protection) kunaweza kuwa na madhira makubwa kwa mtu binafsi, hata kwa Taasisi,
kiuchumi na ustawi wa jamii kiujumla katika Taifa.
Mhe.
Dkt. Mambi aliyasema hayo alipokuwa anatoa mada kwenye Kongamano hilo inayosema
Utatuzi wa Migogoro ya Kazi, Akili Unde na Ulinzi wa Taarifa katika mafunzo ya Usalama
Mahala pa Kazi kati ya Mahakama Kuu ya Tanzania – Divisheni ya Kazi, Taasisi ya
Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) pamoja taasisi za kiserikali
ambazo ni wadau wa mnyororo Mahakama Kazi.
Katika
mafunzo hayo yalitolewa jijini Dodoma katika Ukumbi wa Mikutano wa jengo la
OSHA, na kubeba Kauli mbiu maalum kwa ajili ya kutafakari na kubadilishana
uzoefu juu ya “Nafasi ya Akili Unde (Artificial Intelligence - AI) Mahali pa Kazi
(Mapinduzi na Fursa)”
Mhe. Dkt. Mambi amesema kukosekana kwa ulinzi
wa taarifa kunaweza kuwa na madhara mbalimbali ikiwemo uvujaji wa taarifa na
kupelekea taarifa nyeti kuvuja kama vile taarifa za watu binafsi, taarifa za
kifedha hata kumbukumbu za nyaraka muhimu za kiusalama kwa Taasisi na Nchi kwa
wadukuzi na watu wasiyo ruhusiwa kuzifikia taarifa hizo, matokeo yake inaweza
kuwa, wizi wa mali au taarifa, ulaghai na pengine kupelekea usaliti.
Aidha,
madhira mengine yanaweza kuwa ya kisheria, Mhe. Dkt. Mambi amesema, nchi nyingi
duniani zimeweka mashariti, miongozo, sera na sheria kali za kulinda taarifa
binafsi na pengine mtu anayekwenda kinyume na takwa hilo anaweza kuchukuliwa
adhabu kali, kutozwa faini kubwa na kuburuzwa mahakamani ama kufungiwa maisha
kufanya biashara kwa baadhi ya maeneo dunia.
Vilevile,
Mhe. Dkt. Mambi ameongeza kuwa, kushindwa kulinda taarifa binafsi kunapoteza
uaminifu kwa wateja na washabiki wa biashara husika ambayo mfanyabiashara ama Taasisi
inayoendesha biashara ama mtoa huduma kwa kundi la watu fulani na kusababisha
kupoteza mapato yaliyokuwa yanapatikana.
Amesema
pia kuwa uaminifu ukivunjika ni vigumu tena kujenga taswira ya kampuni ama
taasisi hiyo iliyokuwa ikitoa humuma husika kwa wateja au wananchi waliyokuwa
wakiamini huduma husika.
Ametaadharisha
madhara mengine ya kushindwa kulinda taarifa binafsi inaweza sababisha upotevu
wa mapato kwa taasisi ama kampuni kutokana na fidia kubwa za kisheria ambazo
zinagharimu fedha nyingi, ulaghai wa kutolinda mifumo ya taarifa binafsi na
mifumo ya kibiashara ama kutoa huduma kuto aminika tena na wateja, hilo
linapelekea wateja kugomea kutumia bidhaa za mtoa huduma hiyo na kusababisha
aguko la kiuchumi kwa kampuni au taasisi husika na watu kupoteza kazi na
stahiki husika.
Jaji
Mambi ameongeza kuwa, kama taasisi itashindwa kulinda taarifa binafsi za
wahusika wanaohudumiwa kunaweza kusababisha kupoteza imani na sifa ya taasisi
iliyoijenga muda mrefu kulingana na shughuli za kutoa huduma fulani kwa
wananchi. Hali hiyo inaweza kutangazwa katika vyombo vya habari kote na kupelekea
washindani wa taasisi hiyo kutumia udhaifu huo kuididimiza taasisi hiyo katika
kutoa huduma na kusababisha anguko la kiuchumi katika utoaji huduma kwa
wananchi na kutoiamini tena na taswira yake kupotea kabisa katika ushindani wa
utoaji wa huduma.
Mhe.
Dkt. Mambi ameleza kuwa, kushindwa kulinda taarifa binafsi aidha kwa njia ya
kupitia udukuzi unaosababishwa na kukua kwa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) na mambo kama hayo kunaweza kusababisha anguko la uendeshaji wa taasisi katika
shughuli zake za kila siku. Udukuzi huo unaweza kusababisha upotevu wa
kumbukumbu za mafaili muhimu binafsi ya watu, mawasiliano binafsi na muhimu kwa
njia ya imaili na hifadhidata kumbukumbu za wateja na hivyo kuathiri huduma
zinazotolewa na taasisi.
Aidha Mhe. Dkt. Mambi ameongeza kuwa, kutolinda taarifa binafsi kunaweza kusababisha kupoteza ushindani wa kibiashara kwenye taasisi. Kushindwa kulinda taarifa za taasisi za kibiashara ama mipango ya uzalishaji wa bidhaa za kampuni kunaweza kuwasaidia washidani kuharibu shughuli za taasisi ama biashara taasisi inayofanya hivyo kuharibu uchumi na kuvurunga ustawi wa taasisi na wateja wake.
Ulinzi wa taarifa binafsi iwe kwa mtu binafsi ama taasisi ni muhimu ili kuokoa kupotea kwa mapato katika biashara, taarifa za watu akiwa hai ama amefariki ni lazima zilindwe kwa nguvu zote, taarifa binafsi zinamadhara kiuchumi na kijamii zinaweza kusababisha madhara makubwa katika jamii.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni