Ijumaa, 2 Mei 2025

PICHA ZA MATUKIO MENGINE YA ZIARA YA MAJAJI WASTAAFU WA MAHAKAMA KUU YA TANZANIA

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mstaafu,Mhe. Amir Msumi(kushoto) na Rais wa Chama cha Majaji Wastaafu Tanzania, Mhe. Jaji Thomas Mihayo(katikati)tarehe 30 Aprili, 2025 wakiwa Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Kiaki Nkya(kulia) wakiwa katika Chumba Maalum cha Kutolea Taarifa  mbalimbali za Mahakama  ya     Tanzania nchi nzima (Judicial Situation Room)kilichopo kwenye Jengo la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma tarehe 30 Aprili, 2025.
Mkurugenzi wa Menejimenti ya Usimamizi wa Mashauri wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Desdery Kamugisha (kushoto)akitoa maelezo  kuhusu chumba hicho kinavyofanya kazi ya kutoa taarifa mbalimbali za mashauri ya Mahakama ya Tanzania nchini kwa Majaji hao.

Mkurugenzi wa Huduma za Mahakama ya Tanzania,  Mhe. Kifungu. Mrisho 

Tanzania(aliyenyoosha mkono ) ambaye pia ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania akieleza  jinsi Mfumo  wa TANZLII unavyoweza kusaidia kupata taarifa za  maamuzi na kufanya utafiti wa kisheria.

 

Majaji hao wakipata maelezo ya Kituo ya Huduma kwa Mteja cha Mahakama ya Tanzania kutoka kwa Afisa Utumishi na Kiongozi  wa Timu  Kituo hicho, Bi. Evetha Mboya picha hapo chini.

Rais wa Chama cha Majaji Wastaafu Tanzania, Mhe. Jaji Thomas Mihayo(kushoto) akipokea Taarifa ya Kituo  cha Huduma kwa Mteja  cha Mahakama ya Tanzania  kutoka kwa Afisa Utumishi na Kiongozi  wa Timu  Kituo hicho, Bi. Evetha Mboya .

(PICHA NA MAGRETH KINABO- Mahakama, Dodoma)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni