SALAAM ZA POLE
Jaji
Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma leo tarehe 15 Mei, 2025 majira
ya alasiri amefika nyumbani kwa Marehemu Mhe. William Stephen Mandia, Jaji
Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania eneo la Oysterbay jijini Dar es salaam
kutoa salaam za pole kwa Familia, Ndugu, Jamaa na Marafiki kufuatia Kifo cha
Jaji huyo Mstaafu kilichotokea tarehe 13 Mei, 2025 katika Hospitali ya
Muhimbili jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.
Jaji
Mkuu Mhe. Prof. Juma alipowasili nyumbani kwa Marehemu alipata wasaa wa kusaini
Kitabu cha maombolezo na kutoa salaam za pole kwa familia na wanajamii wa eneo hilo
na kuwatia moyo kutokana na msiba huo na kuwaomba kuwa watulivu na kumuomba
Mungu hasa katika kipindi cha majonzi ya kupotelewa na mpendwa wao.

.jpeg)

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni