Jumatatu, 5 Mei 2025

MAHAKAMA SONGWE WASHIRIKI YAADHIMISHA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI

Na Iman Mzumbwe – Mahakama, Songwe

Wafanyakazi wa Mkoa wa Songwe tarehe Mosi Mei, 2025 walijumuika na wafanya kazi wengine katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani ambayo yalifanyika katika Uwanja wa Chama cha Mapinduzi Vwawa Wilaya ya Mbozi.

Maadhimisho hayo yalianza kwa matembezi ya wafanyakazi kuanzia Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Mbozi na kuelekea katika uwanja wa CCM Vwawa. Taasisi na Idara mbalimbali zilishiriki metembezi hayo na kupokelewa na mgeni rasmi ambaye alikuwa Mkuu wa Wilaya Ileje Mhe. Farida Mgeni aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Songwe Mhe. Daniel Chongolo.

Bi. Farida aliwapongeza wafanyakazi wote kwa kufanya vizuri na kwa umoja wao aidha waliwapongeza wale wote waliofanikiwa kuwa wafanyakazi hodari na alisema kuwa Tuzo walizopewa ziwe chachu ya kufanya kazi vizuri na kwa bidii kwa kuzingatia kanuni, weledi na uaminifu. Serikali ipo sukimamia haki za watumishi na wafanyakazi alisema Mkuu wa Wilaya huyo.

Aidha, Kwa upande wa Mahakama wafanyakazi hodari waliopokea tuzo ni pamoja Mlinzi Mkuu wa Mahakama ya hakimu Mkazi Songwe Bw. Sagala Simfukwe, Mlinzi wa Mahakama ya Wilaya Songwe Bw. Omary Osheni Kihendu, Mlinzi Mahakama ya Wilaya Ileje Bw. Osward Enson Mwashitanda pamoja na Msaidizi wa Kumbukumbu Mahakama ya Wilaya Momba Bw. Heny Japheti Mwakalinga.

Mgeni rasmi huyo katika hotuba yake aliwahimiza wafanyakazi wote kuendelea kuchapa kazi kwa bidii ili kuleta maendeleo ya nchi na amesisitiza waajiri watambue na kuwapa tuzo wanyakazi hodari katika ofisi wanazosimamia. Vilevile alikemea tabia ya baadhi ya waajiri kutoa zawadi hewa kwa wafanya kazi hodari na kuongeza kuwa hali hiyo inarudisha nyuma morali ya kufanya kazi kwa wafanya kazi.

Siku ya wafanyakazi duniani kufanyika kila ifikapo tarehe mosi Mei ya kila mwaka Duniani kote ambapo wafanyakazi hupata fursa ya kuwasilisha changamoto zao kwa mwajiri ili ziweke kupata ufumbuzi ikiwa ni pamoja na suala la upandaji wa madaraja na ongezeko la mishahara. 

 Mgeni rasmi Bi Farida Mgomi akihutubia wafanyakazi na wananchi waliohudhuria katika sherehe hizo za mei mosi katika uwanja ccm Vwawa


watumishi wa taasisi mbalimbali wakiwa katika matembezi kuelekea uwanja wa ccm Vwawa ambako sherehe hizo zilifanyika.

wafanyakazi hodari wa Mahakama Mkoa wa Songwe wakiongozwa na Bw. Sagala Simfukwe wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya sherehe hizo.

Meza kuu ambayo Iliongozwa na mgeni rasmi Bi Farida Mgomi ambaye  ni mkuu wa wilaya ya Ileje.


watumishi wa taasisi mbalimbali wakiwa katika matembezi kuelekea uwanja wa ccm Vwawa ambako sherehe hizo zilifanyika.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni