Na CAREEN INOSHI- Mahakama, Moshi
Watumishi wa Mahakama Kuu Kanda Moshi waliungana na Wafanyakazi
wote wa Mkoa wa Kilimanjaro kuadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani tarehe 1
Mei, 2025, ambayo kimkoa ilifanyika katika Viwanja vya Chuo Kikuu Cha Ushirika
Moshi.
Maadhimisho hayo yalianza na maandamano saa nne asubuhi
kuanzia ofisi za TUCTA Mkoa wa Kilimanjaro na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa, Mhe. Nurdin
Babu, ambaye alikuwa mgeni rasmi.
Wakati wa maadhimisho hayo kulikua na zoezi la ugawaji wa
zawadi kwa Wafanyakazi bora. Watumishi wanne wa Mahakama Kuu Kanda ya Moshi
ambao ni Wanachama wa TUGHE walipatiwa zawadi na mgeni rasmi ambazo ni vyeti
pamoja na pesa taslimu.
Watumishi hao ni Bi.Lightness Mtey (Mahakama ya Wilaya
Rombo), Bi. Junice Ngofi (Mahakama ya Wilaya Mwanga), Bw. Edward Mzava
(Mahakama ya Wilaya Same) pamoja na Bi.Hajira Bundala (Mahakama Wilaya ya Hai).
Aidha, kwa upande wa Watumishi wa Mahakama ambao sio Wanachama
wa TUGHE , Ofisi ya Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Moshi iliandaa zawadi za ufanyakazi
bora na hodari.
Watumishi hao ni Bw. Victor Zakaria (Mahakama Kuu Moshi),
Bi. Regina Venace (Mahakama Kuu Moshi), Bi. Doreen Mwanri (Mahakama ya Hakimu
Mkazi ), Bi. Esther Ikina (Mahakama ya Wilaya Moshi) pamoja na Bi. Sophia Kanje
(Mahakama ya Wilaya Siha).
Sambamba na pongezi hizo, Watumishi pia walikumbushwa kujiunga na vyama vya Wafanyakazi kuendelea kufuata maadili ya kazi.
Mkuu wa Mkoa wa
Kilimanjaro, Mhe. Nurdin Babu ambaye alikua mgeni rasmi akitoa hotuba.
Mtumishi wa Mahakama ya Wilaya Rombo, Bi. Lightness Mtey
akipokea zawadi ya Mfanyakazi bora kutoka kwa mgeni rasmi.
Mtumishi wa Mahakama Kuu Kanda ya Moshi, Bw. Victor
Zakaria akipokea zawadi ya Mfanyakazi bora kutoka kwa Mtendaji wa Mahakama Kuu,
Kanda ya Moshi Bi.Maria Itala.
Habari hii imeghaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni