Jumamosi, 3 Mei 2025

MAJAJI WASTAAFU WAFURAHISHWA NA MAGEUZI YA MAHAKAMA YA TANZANIA

 

Wafurahishwa na kinara wa mageuzi

 

Mtendaji Mkuu asema kila Aprili ya mwaka Majaji Wastaafu kutembelea Makao Makuu

 

Na MAGRETH KINABO -Mahakama, Dodoma

 

Majaji Wastaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania,wamefurahishwa na mageuzi ya miundombinu ya majengo ya Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania na Makao Makuu ya Tume ya Utumishi wa Mahakama, yakiwemo Makazi ya Majaji,na mahakama nyingine mbalimbali nchini,huku wakimpongeza Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof.Ibrahim Hamis Juma kwa usimamizi wake imara katika Mhimili huo. 

 

Kauli hiyo imetolewa tarehe 30 Aprili,2025 na Rais wa Chama cha Majaji Wastaafu Tanzania, Mhe. Jaji Thomas Mihayo,ambaye pia ni Jaji Mstaafu wa Mahakama hiyo, kwa niaba ya  wa Majaji  Wastaafu wenzake walipotembelea  majengo hayo.

 

“Tumefurahishwa na mageuzi yaliyofanyika katika miundo mbinu ya maeneo mbalimbali ya majengo ya  Mahakama ya Tanzania, tumeona jinsi majengo haya yalivyojengwa na kusimikwa mifumo tofauti ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano(TEHAMA) ya  kisasa ambayo inarahisisha utoaji haki kwa wakati kwa wananchi,” alisema Mhe. Jaji Mihayo.

 

Mhe. Jaji Mihayo alipendekeza kwa Jaji Mkuu kuwa Jengo la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania litumike kukuza utalii nchini.

 

Kwa upande wake, Jaji Mkuu Mhe. Prof.Juma aliwaelezea kuhusu  mageuzi hayo yaliyofanyika kwa kuangalia historia ya enzi za ukoloni hadi sasa.

 

Katika hatua nyingine Majaji hao walionekana kufurahia mandhari ya majengo hayo, ikiwemo mifumo ya TEHAMA kwa kuonesha tabasamu kila walipokuwa wakitembelea majengo hayo.

 

Majaji hao pia walitembelea ofisi ya Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, ambapo walipata maelezo ya picha za Majaji Kiongozi wa zamani na shughuli za Mahakama hiyo.

 

Naye Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Prof. Elisante Ole Gabriel alitoa maeleze jinsi Mahakama ilivyofanikiwa kujenga Vituo Jumuishi vya  Utoaji Haki(IJCs) sita na kufanikiwa kuokoa kiasi cha fedha sh. bilioni 3.6.

 

Pia aliongeza kuwa ziara hiyo ya Majaji hao ni ya kwanza kufanyika, hivyo Mahakama itaendelea na utaratibu wa ziara ya namna hiyo kila Aprili kwa mwaka.

 

Mkurugenzi wa Menejimenti ya Usimamizi wa Mashauri wa Mahakama ya Tanzania,Mhe.Desdery Kamugishaalipata wasaa wa kuelezea Chumba Maalum cha Kutolea Taarifa za Mahakama nchi nzima (Judicial Situation Room) kilichopo kwenye Jengo la Makao Makau ya Mahakama ya Tanzaniakinavyofanya kazi ya kutoa taarifa mbalimbali za mashauri ya Mahakama ya Tanzania nchini kwa Majaji hao.

 

Wakati huohuo,Mkurugenzi wa Huduma za Maktaba  ya  Mahakama ya Tanzania, Mhe. Kifungu Mrisho Kariho, ambaye pia ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzaniaaliwaonesha Mfumo  wa Maktaba Mtandao( TANZLII) unavyoweza kusaidia kupata taarifa za  maamuzi na kufanya utafiti wa kisheria.

 

Afisa Utumishi wa Mahakama ya Tanzania na Kiongozi  wa Timu ya Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Mahakama ya Tanzania,  Bi. Evetha Mboya alieleza jinsi kilivyoanzishwa na kinavyofanya kazi, ambapo alisema kina uwezo wa kupokea simu zaidi  30 tofauti kwa wakati mmoja.Pia kina mfumo unaowezesha kupata taarifa mbalimbali za siku, wiki na mwezi, kurekodi mazungumzo na hauna gharama kwa wananchi.


Alifafanua kwamba  maeneo ambayo, sauti za wananchi zinasikika ni mirathi na utekelezaji wa maamuzi.


Mboya aliongeza kuwa  maeneo,ambayo malalamiko yamepungua ni, upatikanaji wa  nakala za hukumu,utoaji wa hati za kimahakama, dhamana, maadili ya Maafisa wa Mahakama na vikao vya Mahakama ya Rufani Tanzania.


Kituo hicho, kimefanikiwa kutembelewa na wageni mbalimbali wa kitaifa na kimataifa kwa ajili ya kujifunza kutoka  Mahakama ya Msumbiji, Uganda, Zanzibar,Maktaba Kuu ya Taifa ya Tanzania, Wizara ya Katiba na Sheria na Jeshi la Polisi.


Majaji hao pia walishiriki kupanda miti ikiwa ni ishara ya kumbukumbu na kuhifadhi mazingira.


 

Picha ya pamoja ya  Majaji hao, wakiwa katika Jengo la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania. 

Picha ya pamoja  ya Majaji hao, wakiwa katika Jengo la Makao Makuu ya Tume ya Utumishi wa Mahakama.


Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof .Ibrahim Hamis Juma, akifurahia jambo.



Naibu Katibu  wa Tume ya Utumishi wa Mahakama(Maadili na Nidhamu), Bi. Alesia Mbuya(katikati)  akisalimiana na Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Julius Mallaba(k
ulia).


Majaji hao, wakiwa katika  chumba cha mikutano cha  Jengo la Makao Makuu ya Tume ya Utumishi wa Mahakama.

Picha ya juu na chini Naibu Msajili Mwandamizi wa Mahakama  Kuu ya Tanzania, Mhe. Sundi Fimbo(kushoto), akiwaongoza Majaji hao, kutembelea Jengo la  Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania.













(Picha na MAGRETH KINABO-Mahakama, Dodoma)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni