Jumapili, 6 Julai 2025

IGP ATEMBELEA BANDA LA MAHAKAMA YA TANZANIA SABASABA

  • Akoshwa na uboreshaji huduma za Mahakama unaoendelea kila uchwao
  • Asisitiza pia amani ya Nchi

Na MARY GWERA, Mahakama-Dar es Salaam

Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Camilius Wambura ameipongeza Mahakama ya Tanzania kwa kuendelea na uboreshaji wa huduma za utoaji haki nchini.

Akizungumza leo tarehe 06 Julai, 2025 baada ya kutembelea Banda la Mahakama ya Tanzania lililopo kwenye Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere vilivyopo Temeke jijini Dar es Salaam, IGP Wambura amekiri kufurahia hatua zaidi iliyopigwa na Mahakama nchini hususani katika uboreshaji wa huduma zake.

“Nimefurahi sana kutembelea banda hili la Mahakama, na mwaka jana nilikuwa hapa, mwaka juzi pia nilikuwa hapa na sisi kama wateja wakuu wa Mahakama tumekuwa tukijifunza mambo mengi hasa mapinduzi makubwa ya matumizi ya TEHAMA yanayofanywa na Mahakama yetu ya Tanzania na mara kwa mara ninapokuja hapa kuna jambo ninajifunza na kwenda kulifanyia kazi,” amesema Mkuu huyo wa Jeshi la Polisi.

IGP Wambura amesema kuwa, alipotembelea banda la Mahakama mwaka jana alijifunza juu ya matumizi makubwa ya Ofisi ya Huduma kwa Mteja ya Mahakama na kukiri kuwa alivutiwa na eneo hilo na kuwezesha pia kuanzia Ofisi kama hiyo katika Jeshi la Polisi.

Amesema kuwa, uanzishwaji wa Ofisi ya Huduma kwa Mteja kwa Jeshi la Polisi umeleta mafanikio makubwa kwa kuwa imewawezesha kupata mirejesho mbalimbali ikiwemo malalamiko kutoka kwa jamii ambayo inawasaidia kuendelea kufanya uboreshaji wa huduma zinazotolewa na jeshi hilo.

Aidha leo baada ya kutembelea banda la Huduma kwa Mteja la Mahakama, IGP Wambura amepongeza uboreshaji zaidi wa huduma zinazotolewa na Ofisi hiyo tofauti na ilivyokuwa mwaka jana alipotembelea.

“Mwaka huu nimepita tena Ofisi ya Huduma kwa Mteja (Call Centre) na nimekuta Mahakama imepiga hatua, sio Call Centre ile niliyoiona mwaka jana na nasi tumejifunza ili tuweze kupiga hatua zaidi kama wenzetu wa Mahakama kwakuwa katika Dunia hii watu hujifunza kwa wenzao,” amesisitiza.

Kadhalika, Mkuu huyo wa Polisi ameikaribisha Mahakama pia kutembelea Banda la Jeshi la Polisi ili nao waweze kujifunza.

Kwa upande mwingine, IGP Wambura amesisitiza wananchi juu ya umuhimu wa kuilinda amani ambayo Tanzania imebarikiwa nayo.

“Kwanza ni fahari kwa Tanzania kuwa na usalama kwa bara la Afrika na Duniani, hivyo niwahahakishie Watanzania kuwa Jeshi la Polisi litaendelea kusimamia ipasavyo usalama na amani iliyopo, hivyo ni vema pia watanzania waendelea kuilinda amani iliyopo," amesisitiza Mkuu huyo wa Jeshi la Polisi.

Viongozi mbalimbali wa Mahakama na Serikali wameendelea kutembelea Banda la Mahakama ya Tanzania lililopo kwenye Maonesho ya Sabasaba yanayoendelea kufanyika hadi tarehe 13 Julai, 2025.

Banda la Mahakama ya Tanzania linapatikana mkabala na Banda la Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ndani ya Viwanja vya (Sabasaba).

Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Camilius Wambura (kushoto) akimsikiliza mtoa huduma kwenye banda la Mahakama la huduma kwa mteja Hakimu Mkazi Mhe. Adrian Richard Msisiri wakati alipotembelea katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Temeke Dar es Salaam.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Camilius Wambura (kushoto) akimsikiliza mtoa huduma kwenye banda la Mahakama la huduma kwa mteja Hakimu Mkazi Mhe. Adrian Richard Msisiri wakati alipotembelea katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Temeke Dar es Salaam.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Camilius Wambura (kushoto) akimsikiliza mtoa huduma kwenye banda la Mahakama la huduma kwa mteja Hakimu Mkazi Mhe. Adrian Richard Msisiri wakati alipotembelea katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Temeke Dar es Salaam.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Camilius Wambura (kushoto) akitoa maelekezo kwa maafisa wa jeshi hilo alipotembelea kwenye banda la Mahakama la huduma kwa mteja katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Temeke Dar es Salaam.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Camilius Wambura (kushoto) akitoa maelekezo kwa maafisa wa jeshi hilo alipotembelea kwenye banda la Mahakama la huduma kwa mteja katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Temeke Dar es Salaam.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Camilius Wambura (kushoto) akisaini kitambu cha wangeni.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Camilius Wambura (kushoto) akipewa maelezo ya namna mifumo ya TEHAMA ya kimahakama inavyofanya kazi na Hakimu Mkazi Mkuu Mhe. Amani Peter Shao kutoka kurugenzi ya Usimamizi wa Mashauri (hayupo pichani).
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Camilius Wambura (kushoto) akipewa maelezo ya namna shughuli za maboresho zilivyorahisisha utoaji haki mahakamani kutoka kwa Mtakwimu wa Mahakama ya Tanzania kutoka Idara ya Mipango Bw. John Magere na  (hayupo pichani).

Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Camilius Wambura akifanya mahojiano na waandishi wa Habari alipotembelea Banda la Mahakama katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Temeke Dar es Salaam.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Camilius Wambura akifanya mahojiano na waandishi wa Habari alipotembelea Banda la Mahakama katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo barabara ya Kilwa Temeke Dar es Salaam.

 

(PICHA NA INNOCENT KANSHA - Mahakama,Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni