Jumamosi, 5 Julai 2025

JAJI MKUU AKUTANA NA MAJAJI, WATUMISHI WA MAHAKAMA KUU DODOMA

Na ARAPHA RUSHEKE-Mahakama Kuu, Dodoma 

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju jana tarehe 4 Julai, 2025 alikutana na Majaji na Watumishi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Dodoma na kufanya naye mazungumzo mafupi.

Mazungumzao hayo yalifanyika katika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Dodoma na kuhudhuriwa na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani na Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Nkya.

Mhe. Masaju amewahi kuhudumu katika Mahakama hiyo kama Jaji wa Mahakama Kuu kabla ya kuteuliwa kuwa Msaidizi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju akisalimiana na watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma katika Kituo Jumuishi chaUutoaji Haki IJC Dodoma mara baada ya kuwasili katika Mahakama hiyo.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju akisaini kitabu cha wageni katika ofisi ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma mara baada ya kuwasili.

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt Mustapher Mohamed Siyani (aliyesimama) akiwasalimia watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju (kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt Julian Masabo.

Meza kuu ikiongozwa na Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju (aliyekaa katikati) kushoto kwake Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani na kulia kwake Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt Juliana Masabo ikiwa katika picha ya pamoja na Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dodoma.

Meza kuu ikiongozwa na Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju (aliyekaa katikati) kushoto kwake Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani na kulia kwake Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt Juliana Masabo ikiwa katika picha ya pamoja na Naibu Wasajili pamoja na Watendaji wa Mahakama ya Tanzania.

Meza kuu ikiongozwa na Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju (aliyekaa katikati) kushoto kwake Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani na kulia kwake Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt Juliana Masabo ikiwa katika picha ya pamoja na na baadhi ya watumishi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Mcheche Masaju akikata keki aliyoandaliwa na watumishi wa Mahakama Kuu Dodoma.

Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama,Dodoma

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni