Na Daniel Sichula – Mahakama, Mbeya
Jaji
wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Barke Sehel afungua kikao cha awali cha
tathmini ya usikilizaji wa mashauri ya rufaa kwa mwaka 2025/2026 katika
Mahakama ya Rufani Kanda ya Mbeya.
Akipokea
taarifa ya tathimini kutoka kwa Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani Tanzania
Mhe. Charles Magese alisema kuwa mashauri 25 yamepangwa kusikilizwa kuanzia
tarehe 21 Julai 2025 hadi 07 Agosti 2025.
Aidha,
akisoma taarifa hiyo Mhe. Magese alifafanua kwamba, Mashauri 12 ni mashauri ya
jinai na 12 ni mashauri ya madai na mashauri yote ni ya mlundikano na shauri
moja ni maombi.
Usikilizaji
wa mashauri hayo ya rufaa utaongozwa chini ya jopo la Majaji watatu akiwemo
Mwenyekiti wa jopo hilo Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Barke Sehel, Jaji
wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Zepharine Galeba na Jaji wa Mahakama ya
Rufani Tanzania Mhe. Amour Khamis
Mara
baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Mhe. Magese, wajumbe walijadili na kutoa
changamoto zinazoweza kujitokeza na namna ya kutatua kabla ya usikilizaji wa
mashauri kuanza ikiwemo wafungwa walioko mbali na mkoa wa Mbeya kufika kwa
wakati mahakamani.
“Mhe.
Jaji, wafungwa wote waliopo mbali na Mkoa Mbeya taratibu zimeshafanyika kabla
ya kuanza vikao jumatatu watakua tayari mkoani Mbeya na tutawafikisha kwa
wakati mahakamani,” alisema Afisa Magereza.
Vilevile,
Afisa Magereza huyo alitoa ombi kwa joto la Majaji wa Rufani kuweza kutoa
hukumu kwa wakati kwa wadaawa waliopo magerezani.
Katika
kikao hicho shauri moja liliombwa kuondolewa na mmoja wa wajumbe waliohudhuria.
“Ni
muhimu kutolea taarifa mapema kwa mashauri ambayo mnataka kuyaondoa kabla
hayajapangiwa usikilizaji kwani hili litasaidia kuondoa na kupanga shauri linguine,”
alisema Mhe. Sehel.
Mhe.
Sehel aliwasisitiza wajumbe wote wakiwemo Mawakili wa Serikali, Maafisa wa
Magereza, Polisi, Mawakili wa Kujitegemea, Ofisi ya Waendesha mashtaka (NPS)
kuwahi kufika kwenye kesi mapema na kuwaambia usikilizaji wa mashauri utaanza
saa 3.30 asubuhi.
Aidha,
kikao hicho kilihudhuriwa na uongozi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya uliyowakilishwa
na Jaji wa Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga, Naibu
Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu, pamoja na
Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Bi. Mavis Miti.
Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Barke Sehel afungua kikao cha awali cha tathmini ya usikilizaji wa mashauri ya rufaani Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya.
Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Charles Magese akitoa taarifa ya usikilizaji mashauri ya Mahakama ya Rufani Kanda ya Mbeya.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni