Na INNOCENT KANSHA-Mahakama
Majaji
wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania, Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Naibu Wasajili wa
Mahakama Kuu na Rufani, Wakurugenzi, wakurugenzi wasaidizi na Wakuu wa Idara na
Vitengo kutoka Mahakama ya Tanzania jana tarehe 20 Julai, 2025 waliungana na
Watumishi wa Mahakama, ndugu, jamaa na marafiki kuuaga mwili wa marehemu Bi.
Sophia Bakari Mohamed aliyekuwa mtumishi wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania
nyumbani kwake katika viunga vya mtaa wa Kikuyu jijini Dodoma.
Awali
akitoa salamu za pole kwa niaba ya Mahakama na kumuelezea Bi. Sophia, Mtendaji
wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Bw. Victor Kategere alimuelezea Mtumishi huyo kuwa
alihudumu Mahakamani kwa takribani miaka 5 na alikuwa muadilifu na mchapa kazi watu
wote walimpenda kwa jitihada zake kazini.
“Mtumishi
wetu Sophia Bakari Mohamed ambaye tulikuwa naye Mahakama, alikuwa mtumishi
ambaye hata sisi wenyewe tulimpenda sana lakini haya masuala mengine
yaliyotokea kama hili ni mambo ambayo wote hatuwezi kuyakwepa. Naamini
linapotokea tukio kama hili mara nyingi mwenzetu kazi yake ameimaliza na safari
yake imefika mwisho,” alisema Mtendaji huyo.
Mtendaji
huyo aliongeza kuwa, kinachotakiwa kuangaliwa wakati tunamsindikiza na
kusherekeka maisha ya mpwenda wetu ni sisi wenyewe kuendelea kutafakari binafsi
na wewe mwenzangu tumejipangaje ili safari yetu iweze kuwa nzuri lakini
pia tuwe na historia njema, mtakumbuka pia kwamba kuna mpendwa wetu Rais
Msataafu aliwahi kusema kwamba, kifo hakikwepeki lakini ni vizuri uwe
umejiandaa ili historia yako itakayo baki iwe historia jema na kuandika kitabu
chema….
Wito
mkubwa katika tukio hili ni sisi wenyewe kujipanga na kutafakari maisha yatu
wenyewe yanavyokwenda tulimpenda sana Sophia wengine tumefanya naye kazi,
wengine wamesoma naye wameshirikiana naye kwenye mambo mengi basi hayo yote
yaliyofanyika ni kwa mpango wa mwenyezi Mungu. Basi kwa pamoja tuendelee
kumuombea ili aweze kupumzika kwa Amani na mwenyezi Mungu aweze kumpokea mahali
pema pepeoni,” aliongeza Bw. Kategere.
Kwa
upande wake, Mchugaji kutoka Kanisa la Kiinjili la kilutheri Tanzania (KKKT)
akitoa mahubiri alisema, matukio ya msiba ya namna kama huo siyo jambo rahisi
kuyapokea kuachana na mtu mliyemzoea ambaye hamtakuwa naye tena katika macho ya
nyama hasa ninyi watumishi wenzake.
Huu
msiba unaumiza kwa sababu ni miaka 29 tu bado mpendwa wetu alikuwa kijana,
kijana wa miaka 12 mpaka 35 bado ana nafasi kubwa ya nguvu kazi kabisa. Tena
yamkini alikuwa na nafasi ya kujiendeleza kielimu ili kuboresha sifa na utukufu
kwenye jamii yetu ya kitanzania na kwenye familia pia, kwa hiyo niendelee kusema
Mungu atutie nguvu sana.
Akifafanua
Mchungaji alisema, neno liliosomwa linasema mwili wa ufufuo katika kristo, ni
kweli misiba inaumiza sana na hata wakati mwingine tunaona kama tumempoteza
vile tu hatuna namna lakini niseme ndugu yetu huyu ameondoka ametangulia kwenye
pumziko la milele, lakini kuondoka kwake ni vigumu kulipokea na kulikubali na
hata watumishi wenzake mnaendelea kuona uwepo wake, ambao sasa haupo pamoja
nanyi.
Mchungaji
ameongeza kuwa, Sura nzima ya waraka huo inagusa juu ya maisha binadamu
yanayotaka kuwe na mahusiano na Mungu ikimaanisha kwamba kifo cha kutengana
ndugu na jamaa siyo mwisho wa kutengana na mahusiano na Mungu bali kinatoa
nafasi ya kutengana na binadamu wengine na ndiyo maana hakizoeleki siku zote,
kinapotokea kinatisha na kinaonekana ni kipya kwenye macho ya nyama.
Aidha, Mchungaji amesema ni muda wa waamini wote kutafakari kwa kina maisha baada ya yale dunia yaani maisha baada ya kifo je waamini mmejipanga vipi kuhusu maisha yenye makazi mapya ambayo ni fumbo kwa kila mmoja wetu, hivyo tuendelee kuamini kuna uzima na ufufuko wa milele.
(PICHA NA INNOCENT KANSHA-Mahakama)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni