Ijumaa, 4 Julai 2025

USIKILIZAJI MASHAURI YA RUFANI MAWAKILI WASISITIZWA KUZINGATIA KANUNI

Na Daniel Sichula- Mahakama, Mbeya 

Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Ferdinand L. Wambali ameongoza kikao cha tathimini (Post session) ya uendeshaji mashauri ya rufaa za Mahakama ya Rufani jijini Mbeya na kutoa rai kwa mawakili kuzingatia kanuni za Rufaa wakati wa usikilizaji wa mashauri ya Rufani.

Aidha, kikao hicho akilijumuisha Jopo la lililoundwa na Majaji Watatu wa Mahakama ya Rufani chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Wambali, huku Majaji wengine wa Mahakama hiyo walikuwa ni Mhe. Gerson J. Mdemu pamoja na Mhe. Latifa A. Mansoor.

Akitoa taarifa ya tathimini ya uendeshaji wa mashauri kwa jopo hilo Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Omary H. Kingwele alisema mashauri hayo yamesikilizwa kwa asilimia themanini na tano (85%) na mashauri 9 yanasubiri uamuzi, huku mashauri 13 yameamuliwa na mashauri 4 ya Rufaa yamehairishwa. Vilevile katika mashauri yaliyoamuliwa mashauri ya jinai ni 6 na mashauri ya madai ni 7.

Akifafanua kuhusu sababu zilizopelekea usikilizaji wa mashauri hayo ya Rufani kufanikiwa kwa 85% Mhe. Kingwele alisema ni kutokana na waadawa wa rufani hizo kufika kwa wakati kipindi cha usikilizaji wa mashauri, mawakili wa wadaawa walifika kwa wakati kwa kipindi chote cha usikilizaji wa mashauri.

Katika taarifa hiyo Naibu Msajili huyo alitoa mapendekezo kwa wadau waliohudhuria kikao hicho kuwa mosi, Mawakili wanatakiwa kujiandaa vyema katika kuwaongoza wateja wao kabla ya kuanza usikilizaji wa mashauri, Pia kuongeza umakini katika uandaaji wa vitabu vya rufaa.

Wakati huohuo wadau kutoka Jeshi la Polisi, Magereza, Mawakili wakijitegemea, Mawakili wa Serikali, Ofisi ya Waendesha Mashtaka walitoa maoni yao pamoja na ushari kwa Mahakama ya Rufani Tanzania.

“Naomba Mhe. Jaji wa Mahakama Rufani hukumu ziwezi kutolewa kwa wakati ilikusaidia watu kupata haki zao mapema” alisema mmoja wa washiriki.

Vilevile kikao hicho kilihudhuriwa na Viongozi wenyeji ambao ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga, Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya Mhe. Said Kalunde, Jaji wa Mahakama ya Tanzania Kanda ya Mbeya Mhe. Victoria Nongwa, Jaji wa Mahakama ya Tanzania Kanda ya Mbeya Mhe. Musa Pomo, Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu, Hakimu Mfawidhi Mkoa wa Mbeya Mhe. Zawadi Laizer, Hakimu Mfawidhi wa Mkoa wa Songwe Mhe. Francis Kisheni, Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Mkazi Mbeya Mhe. Teddy Mlimba pamoja na Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Bi. Mavis Miti.

Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania na Mwenyekiti wa Jopo Mhe. Ferdinand Wambali (katikati) akifungua kikao cha tathimini ya vikao vya Mahakama ya Rufani vilivyofanyika jijini Mbeya (Post session) Majaji wengine wa Mahakama hiyo walikuwa ni Mhe. Gerson J. Mdemu (kushoto) pamoja na Mhe. Latifa A. Mansoor (kulia).

Sehemu ya Viongozi Waandamizi wakifuatilia kikao hicho 

Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya Bi. Mavis Miti sambamba na washiriki wengine katika kikao cha tathimini cha Mahakama ya Rufani Tanzania Kanda ya Mbeya.





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni