Jumanne, 8 Julai 2025

WATUMISHI MAHAKAMA SONGWE WATEMBELEA MAKAO MAKUU, KITUO JUMUISHI DODOMA

Na ARAPHA RUSHEKE - Mahakama Kuu Dodoma

Watumishi wa Mahakama Mkoa wa Songwe hivi karibuni walitembelea Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania pamoja na Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) Dodoma, kujifunza mambo mbalimbali ya kimahakama.

Baada ya kuwasili katika jengo hilo, watumishi hao walipata fursa ya kuonana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mahakama Kuu Kanda, Bw Leonard Magacha.

Akizungumza na watumishi hao katika Makao Makuu ya Mahakama yaliyopo Tambuka Reli Dodoma, Bw. Magacha aliwafahamisha miundombinu ya Mahakama pamoja mambo mengine ambayo yanafanyika katika jengo hilo.  

Ziara hiyo ililenga kujifunza kuhusu utekelezaji wa majukumu ya kimahakama, mifumo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano-TEHAMA, maboresho mbalimbali ya huduma kwa wananchi pamoja na kubadilishana uzoefu katika utendaji kazi wa kila siku.

Watumishi hao walitembelea ofisi mbalimbali ikiwemo chumba cha kunyonyeshea watoto, ukumbi wa mikutano, chumba cha Watoto cha kusubilia, chumba cha mifumo ya TEHAMA pamoja na kituo cha huduma kwa mteja.

Baada ya ziara yao, watumishi hao walionesha kufurahishwa na uboreshaji wa miundombinu ya Mahakama na kuipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Uongozi wa Mahakama ya Tanzania kwa kufanikisha kazi hiyo pamoja na maboresho hayo.

Waliahidi kutumia maarifa waliyoyapata kuboresha huduma kwa wananchi wa Songwe kupitia Mahakama zao.

Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda, Bw. Leonard Magacha (wanne kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi kutoka Mahakama Mkoa wa Songwe walotembelea jengo la Makao Makuu ya Mahakama.

Watumishi kutoka Mahakama Mkoa wa Songwe wakiwa katika picha ya pamoja eneo la Makao Makuu ya Mahakama.

Msanifu wa Majengo wa Makao Makuu ya Mahakama, Bw.Wolfram Mremi akiwapa elimu mbalimbali kuhusu jengo la Makao Makuu watumishi wa Mahakama Mkoa wa Songwe.

Baadhi ya watumishi wa Mahakama Mkoa wa Songwe wakiwa katika moja ya chumba cha watoto kilichopo Makao Makuu ya Mahakama wakati wa ziara hiyo.

Watumishi wa Mahakama Mkoa wa Songwe wakiwa katika chumba cha mifumo kilichopo Makao Makuu ya Mahakama wakisikiliza kwa makini jinsi mifumo inavyofanya kazi kutoka kwa Ofisa TEHAMA, Bw. Richard Matasha (hayuko pichani).

Msanifu wa Majengo wa Makao Makuu ya Mahakama, Bw. Wolfram Mremi akiwapa elimu mbalimbali kuhusu jengo la Makao Makuu watumishi wa Mahakama Mkoa wa Songwe.

Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda, Bw. Leonard Magacha (wasita kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi kutoka Mahakama Mkoa wa Songwe walipotembelea Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) Dodoma.

Watumishi wa Mahakama Mkoa wa Songwe wakisikiliza maelezo kuhusu Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) kutoka kwa Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda, Bw. Leonard Magacha (hayupo pichani).

Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda, Bw. Leonard Magacha akiwaelezea mambo mbalimbali watumishi wa Mahakama Mkoa wa Songwe walipotembelea Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Dodoma (IJC).

Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dar es Salaam.

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni