Alhamisi, 7 Agosti 2025

MAHAKAMA YA RUFANI YAHITIMISHA KIKAO CHAKE JIJINI MBEYA

Na Daniel Sichula – Mahakama, Mbeya

Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Barkel Sahel ahitimisha vikao vya usikilizaji wa mashauri ya rufaani kwa mafanikio mashauri yaliyokuwa yakiendeshwa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya.

Akisoma taarifa ya vikao hivyo Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Charles Magesa alisema kwamba mashauri 24 ya rufaa kati ya 25 yaliyopangwa kusikilizwa yalisikizwa na moja lilihairishwa kwa sababu zilizokua nje ya uwezo wa Mahakama hiyo, katika mashauri 24 yaliyosikilizwa mashauri 22 yametolewa maamuzi na mashauri 2 yanasubiri kutolewa maamuzi.

Mhe. Magesa ameongeza kuwa mafanikio waliyofikiwa ni sawa na asilimia 96 ya mashauri yote yaliyosikilizwa na asilimia 91 ni kwa mashauri 22 yaliyotolewa maamuzi.

Aidha, katika taarifa hiyo iliyotolewa iliainisha changomoto zilizojitokeza katika usikilizaji wa mashauri ya rufani kuwa ni pamoja sababu za rufaa kujirudia rudia na zingine kuchelewa kuwasilishwa.

Kwa upande wa Mashataka changamoto iliyojitokeza ni kushindwa kuleta mashahidi mahakamani hasa kwenye mashauri ya ubakaji na ulawiti kama vile Askari Polisi na Madaktari.

“Watu wa Mashtaka nawasisitiza kuwafikisha mashahidi mahakamani wakati wa usikilizaji wa mashauri ya rufani ili haki iweze kutendeka.” alisema Mhe. Sahel

Mhe. Sahel aliwashukuru wadaawa wote kwa kuweza kufika mahakamani kwa wakati na kwa ushirikiano walioutoa mpaka kufikia mafanikio na malengo ya usikilizaji wa mashauri kwa kiwango cha asilimia 96.

Wajumbe waliohudhuria kikao waliwapongeza Majaji wa Rufani kwa kazi kubwa waliyoifanya ya kusikiliza mashauri hayo yaliyokuwa yamepangwa kusikiliza katika Jopo hilo.

“Waheshimiwa Majaji tunawapongeza sana kwa kazi mliyoifanya, tunaahidi changamoto zote zilizojitokeza tutazifanyia kazi na kuahidi kutojirudia tena kwa vikao vijavyo,” alisema mshiriki kutoka Ofisi ya Mashtaka.

Vilevile, katika kakio hicho kilihudhuriwa na Jaji wa Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga, Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Victoria Nongwa, Majaji wa Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Mbeya Mhe. Musa Pomo,

Wengine walioshiriki kikao hicho ni Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu, Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Bi.Mavis Miti, Mahakimu Mkoa wa Mbeya na Songwe, Mawakili wa Serikali na Wakujitegemea, Afisa Magereza, Askari Polisi pamoja na wawikilishi kutoka ofisi ya Waendesha Mashtaka wa Serikali.

Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Barkel Sahel (katikati) akiendesha kikao cha tathmini ya uendeshaji mashauri ya Rufani kilichoketi Mahakama Kuu jijini Mbeya 

Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Charles Magesa akitoa taarifa ya tathmini ya uendeshaji mashauri hayo.


Sehemu ya wajumbe walioshiriki katika kikao hicho cha mashauri yaliyokuwa yakiendeshwa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya.



Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Victoria Nongwa (kushoto), Majaji wa Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Mbeya Mhe. Musa Pomo (katikati) na Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu wakifuatilia kikao hicho. 


Sehemu ya wajumbe walioshiriki katika kikao hicho cha mashauri yaliyokuwa yakiendeshwa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya.

          

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni