Jumanne, 19 Agosti 2025

WANACHAMA WA TMJA SONGWE WASISITIZWA JUU YA MATUMIZI YA MTANDAO

Na. Iman Mzumbwe – Mahakama, Songwe

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, Mhe. Joachim C. Tiganga alifanya ziara katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Songwe, ambapo ziara hiyo ilikuwa na lengo la kutoa semina juu ya matumizi ya mtandao kwa wanachama wa TMJA katika shughuli za kimahakama pamoja na kutembelea mradi wa Ujenzi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki IJC -Songwe.

Aidha, katibu wa chama cha TMJA Mhe, Komba E. Tagha alisoma taarifa fupi juu ya maendeleo ya chama hicho na aliongeza kwa kusema chama kinajumla ya wanachama 26, ambapo ndani yake kuna wanaume 20 na wanawake 6 na wote hao ni wanachama hai, Mhe, Tagha alitaja malengo makuu ya chama hicho kuwa ni kutoa elimu kwa wanachama na jamii lakini pia kuanglia maslahi ya Majaji na Mahakimu.

Akizungumza na wanachama hao wa TMJA katika ukumbi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Songwe, Mhe, Tiganga aliwakumbusha kuwa malengo makuu ya Mahakama ni kuboresha uelewa wa kisheria, kuimarisha maadili ya kazi na kuhakikisha huduma zinapatikana kwa wakati na usawa kwa wananchi wote.

Aidha mafunzo ya mtandao yaliandaiwa na msaidizi wa sheria wa Jaji kutoka Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Adriano Mtafya ambaye aliwasisitiza na kuwaasa juu ya matumizi sahihi ya mitandao na kuwa taarifa zote zitumwe kwenye barua pepe ili kuepusha matumizi ya karatasi. Afisa huyo pia alitoa mafunzo kuhusu mfumo wa kielektroniki wa usimamizi wa mashauri (e-CMS) Data hubi, mahakama mtandao, ambapo alisisitiza na kutoa rai kwa wanachama hao kuhahikikisha wanaijua mifumo yote ya Mahakama ili kurahisisha namna ya utendaji kazi kwa sababu mhimili huo kwa sasa upo kidigitali zaidi.

Mhe, Tiganga alitembelea pia mradi wa ujenzi wa kituo jumuishi Min IJC Songwe na kukagua maendelea ya utekelezaji wa mradi huo akizungumza mara baada ya kutembelea mradi huo Mhe. Tiganga alisema amefurahishwa na maendeleo mazuri ya mradi kwa hatua waliyofikia ni nzuri tofauti na mwaka uliopita, aidha alimsisitiza mkandarasi wa mradi huo kuongeza juhudi zaidi ya ujenzi ili kufikia malengo mradi huo.

Katika ziara hiyo Jaji Mfawidhi aliambatana na baadhi ya viongozi kutoka Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya akiwemo Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Jaji Victoria Nongwa, Naibu Msajili Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu, Kaimu Mtendaji Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Bw. Alintula Watson Ngalile, Tedy Mlimba kutoka Mahakama ya Wilaya Mbeya, Ayubu shellimo kutoka Mahakama ya Mwanzo Uyole, na Abdulaziz Nchimbi kutoka Mahakama ya Mwanzo Mbalizi.

Mhe, Tiganga alipokelewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya Mbozi Mhe. Nemes L. Chami, Mtendaji wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Songwe Bw. Sostenes Mayoka na Mhe. Magreth Kannonyele Mwenyekiti wa Chama cha Majaji na Mahakimu wanawake Songwe.

Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, Mhe. Joachim C. Tiganga akisaini kitabu cha wageni alipofanya ziara ya kikazi Mahakama ya Mkoa Songwe 

Muonekano wa mradi wa Ujenzi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki IJC -Songwe.









Katibu wa chama cha TMJA Songwe Mhe, Komba E. Tagha akisoma taarifa ya chama kwa Mhe, Jaji Mfawidhi



Naibu Msajili Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu akisaini kitabu cha wageni wakati wa ziara hiyo

Jaji Mfwidhi  wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya Mhe Joachim C. Tiganga akisalimiana na wanachama wa chama cha TMJA Songwe.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni