Jumatatu, 29 Septemba 2025

KITUO CHA HUDUMA KWA MTEJA CHAHIMIZA WATUMISHI KUENDELEA KUTOA HUDUMA BORA

Na. Fredrick Mahava- Mahakama, Sumbawanga

Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Mahakama ya Tanzania kimefanya ziara ya kikazi Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Sumbawanga na kuhimiza watumishi Sumbawanga kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi wanaofika mahakamani, ziara hiyo ilifanyika tarehe 25 September, 2025 ikiwa na lengo la kupokea malalamiko, maoni, mapendekezo kuhusu huduma za Mahakama.

Ziara hiyo ilingozwa na Bw. Yahya Abadalah ambaye aliambana na Shifaa Liwali pamoja Amina Mbaga ambapo walipata wasaa wa kutembelea gereza lililopo Sumbawanga na kupokea malalamiko, maoni, mapendekezo na maulizo kuhusu huduma zinazotolewa na Mahakama.

Aidha, walipata wasaa wa kuongea na wateja waliokuja kupata huduma mahakamani siku hiyo na kupokea malalamiko, maoni, mapendekezo na maulizo kuhusu huduma zinazotolewa na Mahakama.

Vilevile, Kituo hicho cha Huduma kwa Mteja waliweza kufanya kikao na watumishi wa Mahakama Kanda ya Sumbawanga katika ukumbi uliopo Mahakama Kuu Sumbawanga kikao kiliongozwa na Mhe. Deontina Kashaija ambapo waliweza  kupokea malalamiko, maoni, mapendekezo na maulizo kuhusu changamoto za kiutumishi na huduma zinazotolewa na Mahakama.

Naye, Bw. Yahya Abadalah aliwaeleza watumishi baadhi ya kero, malalamiko waliyopokea baada ya kutembelea gereza la Sumbawanga na kutoka kwa wateja waliowakuta mahakamani hapo wakisubiria huduma na kuwataka watumishi kujitahidi kutoa huduma bora.

Bw. Abadalah alitoa salamu za pongezi kwa watumishi wa Mahakama Kanda ya Sumbawanga kwani kero nyingi walizopokea katika mkoa huo zilikuwa siyo za kimahakama bali ni changamoto zinazotokea kwenya mabaraza ya ardhi.

Kwa upande wake, Bi. Shifaa Liwali aliwaeleza watumishi kuwa Kituo cha Huduma kwa Mteja kimeanzisha utaratibu wa kupokea malalamiko, maoni na mapendekezo kupitia mitandao ya simu na Whatsap chatbot kwa namba O752500400. Sambamba na hilo kituo kimeanzisha utaratibu wa kupokea kero zinazohusu watumishi wa Mahakama kupitia namba 07930110002 au Whatsap kwa namba 07930810002.

Aidha, Kaimu Mtendaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga Bi. Irene Mlangwa   alikishukuru Kituo cha Huduma kwa Mteja kwa kufanya ziara hiyo ya kikazi Kanda ya Sumbawanga na kuwataka watumishi kuendelea kutoa huduma bora kwa Wananchi ili kupunguza kero na malalamiko yanayojitokeza

Wakati wa kikao hicho watumishi wa Mahakama Kanda ya Sumbawanga walipata wasaa wa kuuliza maswali, kutoa salamu za pongezi kwa kituo, malalamiko na mapendekezo.

Mhe. Deontina Kashaija akiongoza kikao kati ya Watumishi na Kituo cha Huduma kwa Mteja walipofanya ziara ya kikazi Kanda ya Sumbawanga. 

Mhe. David Mbembela akichangia hoja wakati wa kikao kati ya watumishi na Kituo cha Huduma Kwa Mteja.

Kaimu Mtendaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga Bi. Irene Mlangwa   akizungumza wakati wa kikao.

Watumishi wa Mahakama Kanda ya Sumbawanga wakisikiliza kwa makini wakati wa kikao

Bi. Shifaa Liwali kutoka Kituo cha Huduma kwa Mteja akizungumza wakati wa kikao na Watumishi wa Mahakama Kanda ya Sumbawanga.

Bw. Yahya ABadalah kutoka Kituo cha Huduma kwa Mteja akizungumza wakati wa kikao na Watumishi wa Mahakama Kanda ya Sumbawanga.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni