Na ARAPHA RUSHEKE-Mahakama Kuu, Dodoma.
Watumishi
wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma pamoja na wale wa Mahakama za Wilaya tarehe 26
Septemba 2025 walishiriki katika mafunzo ya Chakula cha Ubongo yaliyolenga
kuongeza uelewa na stadi za kiutendaji.
Mafunzo
hayo yalifunguliwa na Jaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Evaristo
Longopa katika ukumbi wa Mahakama Kuu uliopo Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki
Dodoma (IJC). Sehemu ya washiriki walihudhuria moja kwa moja na wengine kwa
njia ya mtandao kupitia kiungo maalumu (link).
Katika
kikao hicho, mada ya kwanza ilihusu “Jinsi ya Kukabiliana na Vikwazo Mahali
pa Kazi” iliyowasilishwa na Mkurugenzi Msaidizi Anuai za Jamii na Mratibu
wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukizwa kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi, Bi.
Mwanaamini Mtoo.
Mada
ya pili ilikuwa “Maadili katika Utumishi wa Umma” iliyotolewa na Mkurugenzi
Msaidizi wa Idara ya Ukuzaji Maadili kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi, Bi.
Janeth Mishinga.
Akizungumza
wakati wa kufungua mafunzo hayo, Mhe. Dkt. Longopa alisisitiza umuhimu wa
mafunzo ya aina hiyo kwa watumishi wa Mahakama akibainisha kuwa:
“Maadili
na uwezo wa kukabiliana na changamoto kazini ni nguzo kuu za ufanisi katika
kutoa huduma bora kwa wananchi, ni wajibu wa kila mtumishi kuyazingatia haya
kwa vitendo kila siku.”
Kupitia mafunzo hayo, watumishi walipata fursa ya kujifunza mbinu za kukabiliana na changamoto za kikazi pamoja na kuimarisha maadili, jambo linalotarajiwa kuongeza tija na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku.
Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma Mhe. Dkt. Evaristo Longopa (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wakufunzi wa mafunzo hayo. Kulia kwake ni Mkurugenzi Msaidizi Anuai za Jamii na Mratibu wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukizwa kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi, Bi. Mwanaamini Mtoo na kushoto kwake ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Ukuzaji Maadili kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi, Bi. Janeth Mishinga.
Mkurugenzi Msaidizi Anuai za Jamii na Mratibu wa VVU, UKIMWI na Magonjwa Yasiyoambukizwa kutoka Ofisi ya Rais, Utumishi, Bi. Mwanaamini Mtoo akiwasilisha mada wakati wa mafunzo hayo.
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Ukuzaji Maadili kutoka Ofisi ya Rais Utumishi, Bi. Janeth Mishinga akiwasilisha mada wakati wa mafunzo hayo.
Meza kuu ikiongozwa na Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma. Mhe. Dkt. Evaristo Longopa (aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo hayo.
Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni