Alhamisi, 25 Septemba 2025

MAHAKAMA KANDA YA DAR ES SALAAM YAENDESHA MAFUNZO YA UKAGUZI WA MAHAKAMA, UTEKELEZAJI HUKUMU

Na MWANDISHI WETU-Mahakama, Mafia

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Salma Maghimbi amewataka Maofisa Wakaguzi wa Mahakama za Hakimu Mkazi, Mahakama za Wilaya na Mahakama za Mwanzo kuhakikisha wanafanya kazi kwa weledi ili kutimiza lengo la Serikali la kuwahudumia wananchi kwa ufanisi.

Mhe. Maghimbi alitoa wito huo wakati anafungua mafunzo ya ukaguzi wa Mahakama na utekelezaji wa hukumu kwa maofisa wakaguzi katika Wilaya ya Mafia.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Naibu Msajili, Mhe. Beda Nyaki aliwahimiza maofisa hao kufuata mwenendo ya kazi zao pamoja na kufanyia kazi mafunzo walioyapata katika utoaji wa huduma zilizo bora kwa wananchi.

Naye Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kinondoni, Mhe. Jakline Lugemalila, akizungumza kwa niaba ya waliopatiwa mafunzo hayo,  alitoa pongezi kwa Viongozi walioandaa na kuahidi kufanya kazi kwa bidii na kuwajibika kwa kutoa huduma bora.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, Mhe. Salma Maghimbi akisisitiza jambo wakati anafungua mafunzo hayo.


Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kinondoni, Mhe. Jakline Lugemalila akizungumza wakati wa mafunzo hayo.

Sehemu ya washiriki wa mafunzo [juu na picha mbili chini].





Picha za pamoja baada ya ufunguzi wa mafunzo.

Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni