Na. Daniel Sichula – Mahakama, Mbeya
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga afungua
kikao cha awali cha maandalizi ya usikilizwaji wa mashauri ya kesi za mauaji
kwa mwaka 2025/2026 ambapo mashauri hayo yataendeshwa Mahakama Kuu, Kanda ya
Mbeya na Mahakama ya Hakimu Mkazi Songwe.
Akitoa
taarifa ya tathimini Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya
Mhe. Aziza Temu alisema kuwa mashauri 16 yamepangwa kusikilizwa kuanzia tarehe
22 Septemba 2025 ambapo Mashauri 08 yatasikilizwa Mahakama ya Hakimu Mkazi
Songwe mbele ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama kuu Tanzania Kanda ya Mbeya Mhe.
Joachim Tiganga na mashauri 08 yatasikilizwa Mbeya mbele ya Jaji wa Mahakama
Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya Mhe. Victoria Nongwa.
Baada
ya kupokea taarifa ya tathimini kutoka kwa Mhe. Temu wajumbe walijadili juu ya
changamoto zinzoweza kujitokeza na namna ya kuzitatua kabla ya usikilizwaji wa
mashauri kuanza ikiwepo ya mahabusu walioko mbali na sehemu ambako mashauri yao
yatasikilizwa.
Akiwasilisha hoja Afisa Magereza alisema Mhe.
Jaji watu wote wapo mahabusu ila kuna baadhi ya mahabusu wapo Mbeya na mashauri
yao yatasikilizwa Songwe na bado hawajafuatwa.
Akijibu
hoja hiyo Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu kanda ya Mbeya, Mhe. Temu
alisema kuwa “maandalizi yote yameshakamilika na wadaawa wamepelekewa wito wa
kuitwa Mahakamani wakiwemo walioko Songwe na muda wowote kuanzia hivi sasa
mahabusu hao watakuwa wamesha fuatwa kwa ajili ya kusikiliza mashauri yao huko
Songwe”.
Akiwasilisha
taarifa kutoka Ofisi ya waendesha mashtaka mkoa wa Mbeya (NPS), kuwa kwa upande
wao hakuna changamoto yoyote kwenye mashauri yatakayoingia kwenye vikao hivyo.
“Mhe.
Jaji, mashahidi wamepigiwa simu na kupewa wito wa kufika mahakamani na wametoa
ushirikiano wa kutosha na kuthibitisha kuwa wapo tayari kuja kutoa ushahidi
wao” alisema mwakilishi kutoka ofisi ya mwendesha mashitaka mkoa wa Mbeya
(NPS).
Kwa
upande wa Ofisi ya Mwendesha Mashitaka Mkoa wa Songwe waliwasilisha taarifa za
mashauri 08 yanayotarajiwa kusilikilizwa mkoani Songwe na walithibitisha kuwa
hakuna changamoto yoyote na wapo tayari kwa vikao hivyo.
Aidha,
Mawakili wa utetezi nao pia walitoa taarifa zao kuwa nao hawana changamoto
yoyote mandalizi yanaendelea vizuri na wako tayari kwa vikao hivyo kuwasimamia
wateja wao.
“Niwapongeze
washiriki wote, Ofisi ya NPS, Ofisi ya RCO Mbeya na Songwe na Mawakili wa
kujitegemea kwa hatua mlizofikia na kuonesha kuwa hadi sasa hakuna changamoto
yoyote na mupo tayari kwa ajili ya usikilizaji wa mashauri yaliyopo mbele yetu
na kuwasisitiza muda tuliokubalina hapa wa kuanza kusikiliza mashauri yaliyopo
mbele yetu tuuzingatie,” alisema Mhe. Tiganga
“Matarajio
ni kumaliza kesi zote za vikao hivi vilivyoandaliwa na ninawahakikishia kuwa
tumejipanga na kesi zote zitasikilizwa na kumalizika, ninawasisitiza kuwa
wepesi kubadilika kuendana na mazingira ya hali yoyote ya mabadiliko
itakayojitokeza.” Mhe. Jaji Tiganga alisema.
Kikao
hicho kilihudhuriwa na Mtendaji wa Mahakama Kuu Mbeya Bi. Mavis Miti, Mawakili
wa Serikali, Mawakili wa Kujitegemea, Mwakilishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Gereza
Mbeya, Ofisi ya Upelelezi Mkoa wa Mbeya na Songwe na Ofisi ya Waendesha
Mashtaka (NPS) Mkoa wa Mbeya na Songwe.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga (kushoto) akiwa na Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Aziza Temu wakiongoza kikao
cha awali cha tathimini usikilizaji wa mashauri ya mauaji kwa Mahakama Kuu
Mbeya na Mahakama Mkoa wa Songwe.
Sehemu
ya washiriki katika kikao cha awali cha tathimini usikilizaji wa mashauri ya
mauji.
Sehemu
ya washiriki katika kikao cha awali cha tathimini usikilizaji wa mashauri ya
mauji.
Mtendaji wa Mahakama Kuu kanda ya Mbeya Bi. Mavis Miti akiwa mmoja ya washiriki wa kikao hicho
Afisa Magereza akichangia maoni yake katika kikao hicho
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni