TANZIA
Bi. Febronia John Mayala enzi ya uhai wake
Mahakama
Kuu Kanda ya Mwanza inasikitika kutangaza kifo cha mtumishi wake Bi. Febronia
John Mayala ambaye alikuwa Msaidizi wa Kumbukumbu daraja la I kilichotokea
mnamo tarehe 16 Agosti 2025 katika hospitali ya Kamanga Wilaya ya Nyamagana
Mkoa wa Mwanza
Kwa
mujibu wa Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza Bw. Tutubi Mangazeni marehemu
Bi. Febronia aliajiriwa mnamo tarehe 21 Septemba, 2015 katika kada ya Msaidizi
wa Kumbukumbu II.
Baada
ya kuajiriwa alipangiwa Kituo chake cha kwanza cha kazi cha ajira huko Mahakama ya Wilaya
Sengerema na baada ya hapo akahamishiwa Mwanza IJC ambapo alipangiwa Mahakama
ya Wilaya Ilemela na baadaye kuhamishiwa Mahakama ya Hakimu Mkazi mpaka umauti
ulipomfika
Ameajiriwa
na elimu ya Stashahada ya utunzaji wa kumbukumbu (Diploma in Record Management)
katika Chuo cha Utumishi wa Umma tawi la Tabora
Marehemu
Bi. Febronia anatarajiwa kuzikwa Mwanza katika makaburi ya Buhongwa leo tarehe
19 Septemba, 2025.
Bwana ametoa na Bwana ametwaa Jina la
Bwana Lihimidiwe
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni