Na. ARAPHA RUSHEKE – Mahakama Kuu, Dodoma
Watumishi wa Kituo Jumuishi
cha Utoaji Haki Dodoma, pamoja na Mahakama za Mwanzo Dodoma mjini hivi karibuni
wameshiriki mafunzo maalum ya elimu ya mifuko ya uwekezaji yaliyoandaliwa kwa
lengo la kuwajengea uelewa katika eneo la uwekezaji.
Mafunzo hayo yalitolewa
na mtaalamu wa masuala ya uwekezaji kutoka katika mfuko wa uwekezaji [UTT AMIS],
Bw. Ahmed Ismail katika ukumbi wa mikutano wa IJC.
Akizungumza wakati wa
ufunguzi wa mafunzo hayo, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dodoma, Mhe.
Dkt. Juliana Masabo aliwataka watumishi hao kuyazingatia yote watakayofundishwa
kwani yana faida kwa wakati wa baadaye pamoja na wakati wa kustaafu kazi.
“Natamani kila moja
asikilize kwa umakini mambo yote yatakayofundishwa ili tujijengee uelewa katika
masuala ya uwekezaji, naamini elimu itatupa msukumo mkubwa kwa wote kuweza
kujiunga na mifuko hii ya uwekezaji kwa ajili ya faida yako kwa wakati ujao na
wakati wa ustaafu,” alisema Mhe. Masabo.
Kwa upande wake, Bw. Ismail
alibainisha kuwa kuna faida nyingi kwenye uwekezaji ikiwemo fedha kuwa salama,
kutokuwa na tozo zozote kama mabenki na kupata gawio la faida kutokana na faida
ya uwekezaji.
Mafunzo hayo ni mwendelezo wa yale yanayoratibiwa na kutolewa kwa watumishi kwa lengo la kuwajengea uwezo, maarifa na ujuzi katika nyanja mbalimbali za kikazi na maisha yao kwa ujumla.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania,
Kanda ya Dodoma, Dkt. Juliana Masabo (aliyesimama) akitoa neno la ufunguzi wa
mafunzo hayo.
Mwezeshaji wa
mafunzo ya uwekezaji kutoka UTT – AMIS, Bw. Ahmed Ismail alipokuwa akiendesha
mafunzo hayo ya uwekezaji katika mifuko mbalimbali ya uwekezaji.
Sehemu ya
watumishi wa Mahakama walioshiriki katika mafunzo hayo.
Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma



Hakuna maoni:
Chapisha Maoni