Na. Muksini Nakuvamba - Mahakama, Mbeya
Kaimu
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya Mhe. Saidi Kalunde amefanya ziara
ya kutembelea Gereza Kuu Ruanda Mbeya jana tarehe 06 Oktoba, 2025 kwa ajili ya
kujionea shughuli mbalimbali zinazoendelea gerezani hapo pamoja na kusikiliza
changamoto za wafungwa na mahabusu gerezani hapo.
Ziara
hiyo ilianza kwa kupokea taarifa ya Gereza Kuu Ruanda kutoka kwa Kaimu Mkuu wa
Gereza SSP Grace Mbedule ili kufahamu taarifa kamili ya changamoto za wafungwa
na mahabusu gerezani hapo.
Katika
taarifa hiyo alieleza hali za wafungwa na mahabusu waliopo Gerezani hapo,
ambapo kwa sasa kuna jumla ya Wafungwa 681 na Mahabusu 196. Kaimu hiyo Mkuu wa
Gereza SSP Mbedule alieleza changamoto zinazolikabili Gereza Ruanda kwa kusema.
“Mhe.
Jaji mfawidhi, Gereza letu linakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo
ucheleweshwaji wa upelelezi wa kesi suala linalopelekea kuwa na mrundikano
mkubwa wa mahabusu, sambamba na hilo pia kuna Kasha kwa ajili ya Mahakama
mtandao ambalo limekamilika isipokuwa samani zake hazijaletwa ili lianze
kutumika, kwa sasa Mahakama mtandao inaendeshwa ndani ya gereza,” SSP Mbedule
alisema
Taarifa
hiyo ilihitimishwa kwa kumuomba Kaimu Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda ya
Mbeya Mhe. Kalunde kuongeza ushirikiano na vyombo vingine vya haki jinai ili
kukamilisha upelelezi wa kesi kwa wakati ili kukabiliana na changamoto ya
msongamano wa mahabusu gerezani hapo.
Aidha,
Mhe. Kalunde alifanya ukaguzi gerezani hapo kwa kutembelea sehemu za kulala
wafungwa na mahabusu, Zahanati, jikoni na sehemu ya kugawia chakula wafungwa na
mahabusu.
“Niwapongeza
kwa kuwa na sehemu nzuri ya kuandalia chakula na pia alipongeza matumizi ya
nishati ya Gesi na makaa ya mawe kwa kupikia chakula cha wafungwa na mahabusu,”
alisema Mhe. Jaji.
Katika
ziara hiyo Mhe. Kalunde alikutana na Wafungwa na Mahabusu ambao waliwasilisha
changamoto zao kwa Naibu Msajili Mfawidhi Mahakama Kuu Mbeya Mhe. Temu.
Katika
risala iliyosomwa na wafungwa na mahabusu walieleza changamoto zao zinazowakabili
na mapendekezo yao kwa Mhe. Jaji Mfawidhi na naibu msajili mfawidhi “Tunaomba
idadi ya mashauri yanayosikilizwa kuongezwa ili kuturahisishia kupata haki zetu.
Pia tunamuomba Naibu Msajili awe anatutembelea gerezani mara kwa mara ili
kutusikiliza shida zetu,” alisema mfungwa mmoja msomaji wa risala hiyo.
Mhe.
Kalunde vilevile, alitoa fursa kwa Wafungwa na Mahabusu wenye shida binafsi kwake
na kwa Naibu Msajili mfawidhi na wadau wengine wa haki jinai alioambatana kuonana nao kwa utaratibu uliowekwa na
waliweza kusikilizwa shida zao.
Vilevile,
Mhe. Kalunde alitembelea Gereza Kuu Ruanda upande wa Wanawake ambapo kwa upande
huo pia alipokea risala ya Wafungwa na Mahabusu Wanawake ambapo nao
waliwasilisha changamoto zao.
Mhe.
Kalunde pia alitembelea Kasha lilioandaliwa kwa ajili ya kutumika na Mahakama Mtandao
na kujionea miundombinu yake na hatua iliyofikia.
Aidha,
Mhe. Kalunde alihitimisha kwa kutoa shukurani kwa Uongozi wa Gereza, Wafungwa
na Mahabusu wa Gereza la Ruanda. “Nawashukuru kuwa pamoja nasi kuwasikiliza
hoja zenu, tumezichukua na tutazifanyia kazi,” alisema Mhe. Kalunde
Kwa
upande wake Kaimu Mkuu wa Gereza akitoa shukurani zake kwa ujio wa ugeni huo,
kwa kuwa umekuwa na tija kubwa kwao kwa kutoa fursa kadhaa ikiwemo kulipia
ving’amuzi ya televisheni zinazotumiwa na Wafungwa na Mahabusu, kushughulikia
suala la kupunguza mrundikano wa mahabusu na kutoa fursa ya michezo kwa
Wafungwa na Mahabusu wa Gereza kuu Ruanda.
Katika
ziara hiyo Mhe. Kalunde aliambatana na Naibu Msajili Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda
ya Mbeya Mhe. Aziza Temu, Kaimu Mtendaji Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya Bw.
Ibrahim Mgallah, Msimamizi wa Kitengo cha Jinai Mahakama Kuu Mbeya, Mahakimu wakiongozwa
na Hakimu Mkazi Mfawidhi Mahakama ya Wilaya ya Mbeya Mhe. Tedy Mlimba, Ofisi ya
Taifa ya Mashtaka (NPS), Mwenyekiti TLS Chapta ya Mbeya, na wadau wengine wa
Haki jinai.
Kaimu
Mkuu wa Gereza Kuu la Ruanda SSP Grace Mbedule (katikati) akiwa na Kaimu Jaji Mfawidhi
Mahakama Kuu Mbeya Mhe. Said Kalunde (kulia) na Naibu Msajili Mfawidhi wa
Mahakama Kuu Mbeya Mhe. Temu (kushoto).
Kaimu
Jaji mfawidhi Mahakama Kuu Mbeya Mhe. Said Kalunde Akipokelewa na mwenyeji wake
Kaimu mkuu wa gereza, Gereza kuu Ruanda SSP Grace Mbedule alipotembelea
gerezani hapo.
Kaimu
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Mbeya Mhe. Said Kalunde na Naibu Msajili Mfawidhi wa
Mahakama Kuu Mbeya Mhe. Aziza Temu wakikagua miundombinu ya Kasha la mahakama
mtandao.
Kaimu
Jaji mfawidhi Mahakama Kuu Mbeya Mhe. Said Kalunde na Kaimu mkuu wa gereza,
Gereza kuu Ruanda SSP Grace Mbedule wakiwa kwenye matembezi ya ukaguzi Gereza
Ruanda.
Kaimu
Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Mbeya Mhe. Said Kalunde (wa saba kulia) akiwa na
mwenyeji wake Kaimu mkuu wa gereza, Gereza kuu Ruanda SSP Grace Mbedule (kushoto),
Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu Mbeya Mhe. Aziza Temu (wa tano kushoto)
wakiwa mbele ya lango la Gereza kuu Ruanda Mbeya.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni