Na. Iman Mzumbwe – Mahakama, Songwe
Kamati
ya Jaji Mkuu wa Tanzania inayosimamia Masuala ya maendelea ya uboreshaji wa Miradi ya Miudombinu
ya Mahakama tarehe 19 Novemba, 2025 imefanya ziara mkoa wa Songwe kwa madhumuni
ya kukagua na kujioneo hatua za utekelezaji wa Mradi wa ujenzi wa Kituo
jumuishi cha utoaji haki (Intergrated Justice Centre IJC).
Lengo
la ziara hiyo lilikuwa ni kufuatilia maendeleo ya mradi na kufanya tathmini ya
ubora wa kazi, matumizi ya rasimali, utatuzi wa changamoto za utekelezaji
pamoja na kujiridhisha kama mradi unakwenda sambamba na vigezo, viwango na muda
uliopangwa.
Kamati
hiyo iliongozwa na Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. John Ubena aliyeongozana na
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Kanda ya Dar es salaam, Mhe. Salma
Maghimbi, Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu, Kanda ya Dodoma, Mhe. Dkt. Juliana Masabo,
Mtendaji wa Mahakama Kuu Bw. Leonard Magacha na Naibu Msajili Kitengo cha Maboresho
ya Mahakama (JDU) Mhe. John Chacha.
Kamati
hiyo ilitembelea na kukagua sehemu mbalimbali za miradi zikiwemo jengo Kuu la
Utawala, Kumbi za Mahakama na vyumba vya kusikilizia mashauri, sehemu ya mifumo
ya TEHAMA, mfumo wa usalama, miundombinu ya nje na eneo la uzio.
Katika
ukaguzi huo, Kamati ilibaini kuwa maendeleo ya ujenzi huo umefikia takribani
asilimia 73 ya utekelezaji wa mradi, ambapo Mkandarasi wa mradi huo Bw. Andrew
Mpangalala alisema kuwa asilimia zilizobaki kufikia tarehe 31 Disemba, 2025 zitakuwa
zimekamilika na watakabidhi jengo hilo katika mamlaka husika kwa muda huo.
Kamati
ilieleza kuridhishwa na kasi, ubora wa baadhi ya kazi huku ikisisitiza
kuongezwa nguvu katika maeneo machache yanayoonekana kwenda polepole. Aidha kamati hiyo ilitaja baadhi ya
changamoto zinazopaswa kupewa kipaumbele ikiwemo ucheleweshaji wa upatikanaji wa
baadhi ya vifaa vya ujenzi.
Kamati
ya Jaji Mkuu ilitoa maagizo na mapendekezo kwa wadau wote wa mradi akiwemo mkandasi
kuongeza kasi ya utekelezaji ili kufikia muda wa makabidhiano uliopangwa,
msimamizi wa mradi kuimarisha usimamizi wa ubora katika shughuli zote za
finishing na kazi zote zinazoonekana kuwa na changamoto zirekebishwe ndani ya
muda mfupi uliyowekwa na kamati hiyo.
Kamati
ya Jaji Mkuu imepongeza juhudi zinazofanywa na timu ya usimamizi wa mradi
katika Mkoa wa Songwe na imetia moyo hatua ya maendeleo iliyoonekana. Kamati
imesisitiza kuwa mradi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) Songwe ni wa kimkakati
na unatarajiwa kuboresha upatikanaji wa huduma za haki kwa wananchi, hivyo
utekelezaji wake unapaswa kufanyika kwa viwango vya juu kwa uadilifu na ufanisi.
Katika
ziara hiyo, Jaji Mfawidhi Mhakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga alikuwa
ni mwenyeji wa Kamati hiyo ambapo aliambatana na Naibu Msajili Mahakama Kuu
Kanda ya Mbeya Mhe. Judith Lyimo, na Mtendaji wa Mahakakama ya Hakimu Mkazi
Songwe Bw. Sosteness Mayoka.
Kamati ya Jaji Mkuu wa Tanzania inayosimamia Masuala ya maendelea ya uboreshaji wa Miradi ya Miudombinu ya Mahakama wakiwa kwenye picha ya pamoja na timu ya wakandarasi wanaojenga jengo la kituo jumuishi cha utoaji haki mkoani songwe.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga akiwakaribisha Kamati
ya Jaji Mkuu ya miundombinu na kutoa taarifa fupi ya mradi wa ujenzi wa kituo
hicho katika Ofisi ya Hakimu Mkazi Mahakama Songwe.
Kamati
ya Jaji Mkuu ya Miundombinu wakikagua eneo la ujenzi wa mradi wa kituo jumushi
Songwe
Mkandarasi
wa ujenzi wa mradi Bw. Andrew Mpangalala akieleza juu ya maendeleo ya ujenzi mradi
huo ulipofikia
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni