- Amsisitiza Mkandarasi kuongeza bidii kukamilisha mradi huo
Na NAUMI SHEKILINDI, Mahakama-Simiyu
Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Kiaki Nkya amekiri kuridhishwa na maendeleo ya Mradi wa Ujenzi wa Jengo la Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) Simiyu ambao ulikuwa umefikia asilimia 92 hadi kukamilika kwake wakati alipotembelea Mradi huo.
Hivi karibuni, Mhe. Nkya alitembelea Mradi wa Ujenzi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki kinachojengwa Mkoani Simiyu ili kujionea maendeleo ya ujenzi wa Kituo hicho.
Baada ya ukaguzi, Msajili
Mkuu alimsisitiza Mkandarasi kuongeza bidii kwa kumalizia asilimia zilizobaki ili kuweza
kuanza matumizi ya jengo hilo mapema iwezekanavyo.
Naye
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Simiyu, Mhe. Martha Mahumbuga
alimkaribisha Msajili Mkuu na kumsomea taarifa ya utendaji kazi katika Mkoa
huo.
Aidha, Msajili Mkuu alionesha kufurahishwa na ushirikiano uliopo baina ya ‘Judicial na Non-Judicial Officers’ Mkoani humo, “nimependa namna mnavyofanya kazi kwa ushirikiano na hii imejidhihirisha hata kupitia taarifa yenu mlionisomea, hongereni sana Simiyu,” alisema Mhe. Nkya.
Msajili Mkuu aliwashukuru watumishi wa Mahakama Simiyu kwa ukaribisho mzuri alipotembelea Mahakama hiyo.
Muonekano wa Jengo la Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) Simiyu lililopo katika hatua za mwisho za ujenzi wake.
(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)



Hakuna maoni:
Chapisha Maoni