Jumatano, 26 Novemba 2025

MTENDAJI MKUU AKOSHWA NA JUHUDI ZA BANKI YA DUNIA KATIKA MABORESHO

Na. INNOCENT KANSHA - Mahakama

Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Prof. Elisante Ole Gabriel leo tarehe 26 Novemba, 2025 jijini Dodoma amekutana na kufungua Kikao cha ujumbe wa Benki ya duania uliokuja nchini kwa ajiri ya kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na Mahakama ikiwemo ujenzi wa Vituo Jumuishi vya Utoaji Haki vinavyoendelea kujengwa katika mikoa tisa nchini ikiwa ni awamu ya mwisho ya ukaguzi kuelekea hatua za ukingoni.

Vituo hivyo vinavyojengwa katika mikoa mbalimbali nchini na ambavyo vipo katika hatua tofauti tofauti kuanzia mkoa wa Lindi, Songea kwa asilimia 77, Njombe, Songwe, Katavi kwa asilimia 85, Singida, Geita kwa asilimia 94, Simiyu kwa asilimia 95 na Pemba ikiwa ni sehemu ya kudumisha Muungano.

“Uongozi wote wa Mahakama unayofuraha kwa ushirikiano ambao unatolewa na Banki ya Dunia katika kuhakikisha miradi ya maboresho inaendelea vizuri na mambo yote mazuri yanayofanyika ni kutokana na ushirikiao wenu wa dhati wa hali na mali. Pia nichukue fursa hii kuishukuru time ya Maboresho ya Mahakama kwa kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha miradi ya maboresho ya ujenzi wa miundombinu inakamiliaka ifikapo Desemba 31, 2025,” ameongeza Mtendaji Mkuu.

Prof. Ole Gabriel amekiri kupokea ushirikiano wa asilimia 100 kutoka kwa Ujumbe huo na kusema Mahakama imejizatiti kama ilivyoahidi mwezi wa Pili mwaka huu walipokutana na kujadili kama kweli miradi yote itakamilika kwa wakati uliopangwa. Mahakama bado ipo makini kuhakikisha kwamba inasimamia miradi hiyo hasa kipindi cha mwishoni mwa kukamilishwa miradi yote iliyoanzishwa katika awamu ya pili ya ujenzi Mahakama haitalegalega hata kidogo.

Aidha, Mahakama itaendelea kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha kwamba mambo yote yanakamilika kwa wakati uliopangwa, niwahakikishie Banki ya Dunia kwamba, natoa shukrani zangu kwa Timu ya ndani inayotekeleza miradi hiyo ikiongozwa na Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Dkt. Angelo Rumisha.

Kwa upande wake, Kiongozi wa Msafara wa Benki ya Dunia Bi. Christine Owuor, amepongeza kasi ya maendeleo ya ujenzi wa majengo ya Vituo Jumuishi vya Utoaji Haki nchini kwani kwa sasa hatua ni zuri ukilinganisha na miezi sita ya nyumba hali haikuwa nzuri sana.

“Tulikuwa hapa nchini mwezi wa tisa, 2025 katika mwendeleo za ziara ukaguzi wa miradi ya Banki ya Dunia inayotekelezwa na Mahakama hii ni ziara ya mwisho ya utekelezaji wa ukaguzi wa miradi hii kabla haijafika mwisho mwezi Desemba 31, 2025,” amesema Bi. Christine.

Aidha, ameongeza kuwa, malengo ya mradi hajabadilika na kumekuwa na majadiliano mazuri kati ya Banki hiyo na wataalum wa miradi ili kufanikisha matokeo chanya ya mradi, ikiwa ni pamoja na kutekeleza maelekezo yalifikiwa katika ziara iliyopita.

“Ziara hii inaweza kuwa ya kipekee kwa sababu tutahitaji kufikiria na kutafakari namna bora tutakavyo hitimisha miradi kwa ufanisi, tunahitaji kupata ripoti nyingi za uwajibikaji na utekelezaji wa miradi zilizokamilika ili tuweze kukamilisha miradi kwa wakati ndani ya siku mbili ya ziara,” amesema Mkuu huyo wa Msafara.

Aidha, Bi. Christine amesema kuna vitu ambavyo Mahakama ya Tanzania imeviendeleza na kuvisimamia kikamilifu kwa kipindi cha miaka yote 9 kama Chumba cha Ufutailiaji na Taarifa za Utendaji wa Mahakama (Judiciay Situation Room) ambayo ni mfano ambayo watu wanatoka nje kuja kujifunza na inavofanya kazi, hii ikiwa baada ya Mahakama kwenda kujifunza nchini Kazakhstan, kitu kingine kulizishwa kwa huduma kwa mteja (court services satisfaction) imepanda kwa kiwango kikubwa.

Mfumo wa Usimamizi wa Mashauri ya Mahakama kwa Elektroniki (Electronic Case Management System) hilo ndiyo eneo lililoleta mapiduzi makubwa ya utendaji wa mahakama hasa kuchakata takwimu, kusajili mashauri ni maeneo ya kupigiwa mfano na nchi zimekuja kujifunza namna ya uendeshaji, IJA e- learning Platform, baklong clearance hiyo ni maeneo ya mfano.

“Kuna maeneo yanaendelea kufanya vizuri kwenye miradi inayoendelea ya ujenzi kama Pemba, Geita, Simiyu pamoja na Katavi na maeneo mengine ambayo tulikuwa tunayatilia shaka utekeleza wake wa miradi yanaendelea vizuri na yanaridhisha.  Hatukuweza kutembelea maeneo yote safari hii lakini kutokana na ripoti ya maendeleo ya miradi yuyopewa tumefurahishwa nayo,” amesisitiza Bi. Christine.

Vilevile, Bi. Christine ameongeza kuwa, Ujumbe unatambua kuwa fedha zote za mradi zimekishwa kutolewa ili kukamilisha utekelezaji wa miradi kwa miezi hiyo iliyobakia kwa maeneo ambayo bado, Ujumbe hautegemei kurudishwa kwa fedha yoyote katika kutekeleza shughuli zilizobaki kama ununuzi wa magari kuhakikisha yanaletwa kwa wakati.

“Tumekuja kwenye ziara hii tukiwa na furaha kwa kuona kwamba Mahakama ndani ya kipindi cha miezi sita Mahakama imefanya kazi kubwa kutoka pale tulipokuwa tukiomba mkopo wa awamu ya pili kufikia hapa tulipo, tuna toa shukrani zetu kwa timu ya Mahakama na timu ya Banki ya Dunia kwa kuhakikisha tunafanikisha kile tulichokuwa tunakitarajia,” ameongeza Bi. Christine.

Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Prof. Elisante Ole Gabriel akiwa kwenye picha ya pamoja na Ujumbe wa Banki ya Dunia pamoja SO-Owners wa mradi wa Maboresho ya Mahakama.

Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Prof. Elisante Ole Gabriel akielezea jambo wakati wa kufungua kikao cha ujumbe wa Banki ya Dunia leo tarehe 26 Novemba, 2025 IJC jijini Dodoma kulia kwake ni Kiongozi wa Msafara wa Benki ya Dunia Bi. Christine Owuor

Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Prof. Elisante Ole Gabriel (kushoto) akimsikiliza Kiongozi wa Msafara wa Benki ya Dunia Bi. Christine Owuor akisema jambo wakati wa kufungua kikao cha ujumbe wa Banki ya Dunia leo tarehe 26 Novemba, 2025 IJC jijini Dodoma kulia ni Mtaalum kutoka Benki ya Dunia Bw. Benjamin Mtesigwa. 

Sehemu ya wajumbe waliohudhuria ufunguzi wa kikao cha ujumbe wa Banki ya Dunia

Sehemu ya wajumbe waliohudhuria ufunguzi wa kikao cha ujumbe wa Banki ya Dunia


Sehemu ya wajumbe waliohudhuria ufunguzi wa kikao cha ujumbe wa Banki ya Dunia

Sehemu ya wajumbe waliohudhuria ufunguzi wa kikao cha ujumbe wa Banki ya Dunia



Sehemu ya wajumbe waliohudhuria ufunguzi wa kikao cha ujumbe wa Banki ya Dunia


Sehemu ya wajumbe waliohudhuria ufunguzi wa kikao cha ujumbe wa Banki ya Dunia

Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Prof. Elisante Ole Gabriel akiwa kwenye picha ya pamoja na Ujumbe wa Banki ya Dunia pamoja SO-Owners wa mradi wa Maboresho ya Mahakama



Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Prof. Elisante Ole Gabriel akiwa kwenye picha ya pamoja na Ujumbe wa Banki ya Dunia walipofika kukagua miradi ya Maboresho ya Mahakama.

(Picha na INNOCENT KANSHA- Mahakama)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni