Ijumaa, 28 Novemba 2025

WATUMISHI KANDA YA MWANZA NA MUSOMA WAAGA MWILI WA MAREHEMU ABRIEL EZEKIEL LAZARO

Na. REHEMA AWET – Mahakama, Mwanza

Mwili wa marehemu Abriel Ezekiel Lazaro aliyekuwa Dereva wa Mahakama ya Wilaya Bunda umeagwa katika hospital ya Bugando mkoani Mwanza. Baada ya zoezi la kuaga mwili huo wa marehemu ulisafirishwa kuelekea mtaa wa Nzasa Kata ya Chanika Wilaya ya Ilala jijini Dar es salaam kwa ajili ya maziko.

Akizungumza kwa niaba ya Mahakama ya Tanzania Kaimu Jaji Mfawidhi Mhe. Kassim Robert alitoa pole kwa wafiwa, familia, ndugu, jamaa na marafiki waliohudhuria katika zoezi la kuaga mwili wa marehemu Abriel.

Aidha, aliwakumbusha waombolezaji hususani watumishi wa Mahakama kuwa “kifo cha mtumishi mwenzetu kiwe chachu ya kuchapa kazi kwa bidii na uwadilifu huku tukimtanguliza Mungu mbele katika kutekeleza majukumu yetu kwani hatujui siku wa saa,” alisema Jaji huyo.

Naye, Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza Bw. Tutubi Mangazeni alieleza namna ambavyo Mahakama imeshiriki katika taratibu zote za kushughulikia maziko ya mtumishi huyu ikiwemo kuaga mwili wa marehemu, kuusafirisha na baadaye kuupumzisha kwenye nyumba yake ya milele huko jijini Dar es Salaam tarehe 28 Novemba, 2025. Aliongeza kuwa, Mahakama Kanda ya Mwanza na Musoma zimetuma wawakilishi katika maziko haya.

Katika zoezi la kuaga mwili wa marehemu liliongozwa na Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama ya Kuu Kanda ya Mwanza Mhe. Kassim Robert, Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza Mhe.  Emmanuel Ngigwana, Jaji wa Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi Mhe. Godfrey Ntemi Isaya, Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza Mhe. Crisencia Kisongo, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Butiama Mhe. Judith Semkiwa, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Nyamagana Mhe. Ramla Shehagilo, Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza Bw. Tutubi Deo Mangazeni, Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Musoma Bw. Leonard Maufi, na watumishi wengine wa Mahakama Kanda ya Mwanza na Musoma.

Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi Mhe. Godfrey Isaya  akiaga mwili wa marehemu Abriel Lazaro

Sehemu ya waombolezaji wakiwa wamebeba mwili wa marehemu mara baada ya zoezi la kuaga kukamilika.

Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza Mhe. Kassim Robert (wa pili kulia), Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza Mhe. Emmanuel Ngigwana (wa tatu kulia), Jaji wa Mahakama Kuu Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi Mhe. Godfrey Isaya (wa pili kushoto), Naibu Msajili Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza Mhe. Crisencia Kisongo (wa kwanza kulia), Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza Bw. Tutubi Deo Mangazeni (wa kwanza kushoto), na Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Musoma Bw. Leonard Maufi (wa tatu kushoto) wakizungumza baada ya zoezi la kuaga mwili wa marehemu kumalizika.

Sehemu ya waombolezaji wakiwa wamebeba mwili wa marehemu mara baada ya zoezi la kuaga kukamilika.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni