Na. Daniel Sichula – Mahakama, Mbeya
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Mbeya Mhe. Joachim Tiganga aliwaongoza
watumishi wa Mahakama Kuu Kanda hiyo kutembelea Hifadhi ya Taifa ya wanyama
pori ya Ruaha (RUAHA NATIONAL PARK) iliyopo mkoani Iringa.
Aidha,
Mhe. Tiganga akielezea lengo la Safari hiyo kwa watumishi wa Mahakama Kuu Kanda
ya Mbeya alisema, “Watumishi wenzangu tukiwa hapa tunafurahia utendaji wetu wa
kazi na kufikia malengo yetu kwa mwakan huu, kwa kushirikiana na uongozi chini ya
Mtendaji wa Mahakama Kuu Mbeya tukaona inafaa kufanya jambo hili kwa
kupongezana na kuweza kurudi na hali mpya kazini,” alisema Mhe. Tiganga.
Vilevile,
Mhe. Tiganga aliongeza kuwa, hiyo ni fursa ya kukuza utalii wa ndani na kujifunza
jinsi wanyama wanavyoishi na kuona mazingira yao ya kila siku, ikiwa ni pamoja
na kubadili mazingira ya watumishi kutumia muda mwingi maofisini kuwatumikia
wananchi.
Katika
safari hiyo ya kitalii Majaji wengine wa Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Mbeya
walioungana na watumishi wa Mahakama Kuu hiyo ni pamoja na Mhe. Said Kalunde,
Mhe.Victoria Nongwa, Naibu Msajili Mfawidhi Mhe. Aziza Temu pamoja na Mtendaji
wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Bi Mervis Miti.
Picha
na matukio mbalimbali ya watumishi wa Mahakama Kuu Mbeya wakiwa katika Hifadhi
ya Wanyama Pori Ruaha.
Picha
na matukio mbalimbali ya watumishi wa Mahakama Kuu Mbeya wakiwa katika Hifadhi
ya Wanyama Pori Ruaha
Picha na matukio mbalimbali ya watumishi wa Mahakama Kuu Mbeya wakiwa katika Hifadhi ya Wanyama Pori Ruaha.
Picha
na matukio mbalimbali ya watumishi wa Mahakama Kuu Mbeya wakiwa katika Hifadhi
ya Wanyama Pori Ruaha.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Mbeya katikati akiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya.
Watumishi
wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya wakifurahia jambo walipotembelea Hifadhi ya Taifa ya wanyama pori ya Ruaha
(RUAHA NATIONAL PARK) iliyopo mkoani Iringa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni