Na NAUMI SHEKILINDI, Mahakama-Simiyu
Hivi
karibuni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Simiyu, Mhe.
Wilbert Chuma amekaribishwa na watumishi wa Mahakama mkoani humo akitokea
Mwanza ikiwa ni mara ya kwanza kufika katika Kituo hicho tangu alipoteuliwa
kuwa Jaji Mfawidhi wa Kanda hiyo mpya.
Itakumbukwa
kuwa, Mahakama Kuu Kanda ya Simiyu ilitangazwa kuwa Mahakama Kuu kwa tangazo la Serikali
na.690 la 2025 kuanza kutoa huduma kuanzia tarehe 02 Januari, 2026.
Watumishi
Mkoani Simiyu wakiongozwa na Kaimu Naibu Msajili, Mhe. Martha Mahumbuga pamoja
na Mtendaji wa Mahakama Kuu Simiyu, Bw. Gasto Kanyairita walimkaribisha Jaji
Mfawidhi huyo kwa furaha kubwa ikiwa ni pamoja na kumuahidi kufanya kazi kwa
uadilifu, weledi na uwajibikaji.
Aidha,
Mhe. Chuma alitembelea jengo jipya la Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC)
Simiyu na kujionea muonekano wa jengo hilo pamoja na samani za kisasa zilizomo ndani
ya jengo hilo.
Kadhalika,
Jaji Mfawidhi huyo alipata nafasi ya kuongea na watumishi wa Mahakama Kuu Kanda
ya Simiyu (IJC) na kuwasisitiza kuwa na ushirikiano katika kazi, kutoa huduma
bora kwa wateja wa nje na ndani, vilevile kila mtumishi anatakiwa kuyatambua
majukumu yake ili kuweza kufikia malengo na Dira ya Mahakama.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Simiyu, Mhe. Wilbert Chuma akisaini kitabu
cha wageni katika Ofisi ya Kaimu Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Simiyu alipowasili katika Mahakama hiyo hivi karibuni.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Simiyu, Mhe. Wilbert Chuma (wa kwanza kulia) na viongozi wengine wakikagua ubora wa samani katika chumba cha mafunzo ndani ya IJC Simiyu.
(Habari hii imehaririwa na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)






Hakuna maoni:
Chapisha Maoni