Na. MUKSINI NAKUVAMBA - Mahakama Mbeya.
Mahakimu
Wakazi wa Mahakama mkoani Mbeya wametoa elimu kupitia Kituo cha Radio Baraka Fm
ikiwa ni sehemu ya kuuelisha Umma juu ya masuala mbalimbali ya kisheria na
uwepo wa maadhimisho ya siku ya sheria nchini kwa mwaka 2026.
Elimu
hiyo ilitolewa tarehe 28 Januari, 2026 na Mahakimu Wakazi wawili, Wasaidizi wa
Sheria wa Majaji kutoka Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya ambao ni Mhe. Alvin Juae,
Mhe. Adriano Mtafya na Mhe. Ayubu Shelimo.
Akizungumzia
Kaulimbiu ya siku ya sheria nchini Mhe. Ayubu Shelimo alisema mwaka huu
Mahakama inatumia kaulimbiu isemayo “Mchango wa Mahakama katika ustawi na
maendelelo ya Taifa” itakayotumika siku ya sheria nchini na siku ya kilele cha
maadhimisho ya siku ya sheria nchini kwa mwaka 2026, ambayo maadhimisho hayo
yatafanyika siku ya Jumatatu ya tarehe 02 Februari, 2026.
Aidha,
Mhe. Shelimo aliongeza kuwa, kabla ya kufikia kilele cha siku ya sheria nchini Mahakama
Mkoa wa Mbeya umeandaa matukio kadhaa yatakayoambana na siku hiyo ikiwa ni pamoja
na kufanya matendo ya huruma kwa kutembelea Kituo cha kulelea Watoto yatima cha
NURU kilichopo Uyole Mbeya, tukio litakalofanyika siku ya tarehe 30 Januari
2026.
Aliongeza
kuwa, kutakuwa na Bonanza la michezo mbalimbali linalotarajiwa kufanyika siku
ya Jumamosi tarehe 31 Januari, 2026 katika viwanja vya Chuo Kikuu TEKU na
hatimaye sherehe rasmi za kilele cha siku ya sheria nchini siku ya tarehe 02
Februari, 2026 katika viwanja vya Mahakama Kuu Mbeya.
Vilevile,
Mhe. Shelimo aligusia Mikakati ya Mahakama ya Tanzania katika kufikia lengo Kuu
la Dira ya Maendeleo ya Taifa ambayo inaenda sambamba na kusogeza huduma za Mahakama
hadi ngazi ya Kata, kuboresha miundombinu ya TEHAMA, kuimarisha uwazi na
uwajibikaji, kufanya maboresho ya sheria ngumu zilizopitwa na wakati na
kuboresha huduma za Mahakama kupitia mpamgo wa matumizi ya Mahakama
inayotembea.
Kwa
upande wake, Mhe. Adriano Mtafya alizungumzia kuhusu matumizi ya TEHAMA
yalivyosaidia kuborsha shughuli mbalimbali za Mahakama na kuchochea maendeleo
ya Taifa, akifafanua kuhusu faida za TEHAMA alisema inarahisisha ufunguaji wa
mashauri na usikilizwaji wa mashauri kupitia njia ya mtandao na pia aligusia matumizi
ya Mahakama Inayotembea katika kuboresha shughuli za Mahakama ambapo kwa Kanda
ya Mbeya zaidi ya mashauri 100 yamefunguliwa na kusikilizwa hadi kumalizika kupitia
Mahakama inayotembea kwa mwaka 2025.
Naye,
Mhe. Alvin Juae aliongeza kuwa, mchango wa Mahakama ya Tanzania katika
kuboresha maendeleo na kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050,
ambapo alisema kuwa maboresho ya shughuli mbalimbali za kimahakama
zinawawezesha wanachi kufuatilia mashauri yao kwa njia ya mtandao na kutokupoteza
muda mwingi mahakamani.
Mara
baada ya Mahakimu hao kumaliza kutoa elimu hiyo kuhusu Siku ya Sheria nchini,
kipindi kilihitimishwa kwa Mtangazaji kuruhusu kuuliza maswali, ambapo
wasikilizaji waliuliza maswali mbalimbali kuhusiana na elimu iliyotolewa ili
kupata ufafanuzi wa kina hoja mbalimbali.
Mahakimu
Wakazi wa Mahakama Mbeya wakiwa njie ya Studio za Baraka FM Mbeya, Kushoto ni
Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Mbeya Mjini Mhe. Ayubu Shelimo, Katikati ni
Hakimu Mkazi Mahakama Kuu Mbeya Mhe. Adriano Mtafya ambaye ni msaidizi wa
sheria na Kulia ni Hakimu Mkazi Mahakama Kuu Mbeya Mhe. Alvin Juae ambaye pia
ni msaidizi wa sheria.
Mahakimu Wakazi wa Mahakama Mbeya wakiwa Studio za Baraka FM Mbeya wakitoa elimu kwa umma, kushoto ni Hakimu Mkazi Mahakama ya Mwanzo Mbeya Mjini Mhe. Ayubu Shelimo, kulia ni Hakimu Mkazi Mahakama Kuu Mbeya Mhe. Adriano Mtafya ambaye ni msaidizi wa sheria na katikati ni Hakimu Mkazi Mahakama Kuu Mbeya Mhe. Alvin Juae ambaye pia ni msaidizi wa sheria.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni