Na. HABIBA MBARUKU & JAMES BUSANYA, Mahakama-Dodoma
Msajili
Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Eva Nkya leo tarehe 22 Januari, 2026
amefungua mafunzo kwa Maafisa Mirejesho wa Kituo cha Huduma kwa Mteja katika Ukumbi
wa Chumba Maalumu cha Mifumo ya Utoaji Taarifa (Judiciary Situation Room) kilichopo
Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma.
Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo Mhe.
Nkya amesema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo watumishi wote
wanaotekeleza majukumu yao katika Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Mahakama ya Tanzania
(Judiciary Customer Service Center zamani Judiciary Call Centre) katika matumizi
ya mfumo ulioboreshwa wa mawasiliano na mteja, mfumo ambao
ulianza kutumika katika toleo la kwanza ambao sasa umeboreshwa kwa kiwango
kikubwa hadi kufikia toleo la nne.
Mhe.
Nkya ameongeza kuwa maboresho hayo yametokana na uzoefu wa matumizi ya mfumo wa
awali pamoja na tathmini ya mahitaji ya kiutendaji ili kuongeza ufanisi na
kurahisisha upatikanaji wa huduma ya mawasiliano kwa wakati.
“Maboresho haya yametokana na uzoefu
wa matumizi ya mfumo wa awali pamoja na tathmini ya kina ya mahitaji ya
kiutendaji kwa lengo la kuongeza ufanisi, ubora wa huduma na kurahisisha
mawasiliano kati ya Mahakama na wananchi,” amesema Mhe. Nkya
Aidha, Msajili Mkuu ameeleza kuwa, mfumo wa toleo la
nne umeongezewa huduma mbalimbali ikiwemo kuunganishwa na WhatsApp Chatbot,
hatua inayolenga kuisogeza Mahakama karibu zaidi na wananchi kwa kuwafikia
kupitia majukwaa wanayotumia kwa wingi katika maisha ya kila siku.
Ameeleza kuwa tofauti na awali, mfumo huo sasa
unaweza kutumika popote bila kuathiri utoaji wa huduma, hali itakayosaidia
kuongeza ufanisi wa kazi na mwendelezo wa huduma kwa wananchi wakati wote.
Mhe. Nkya ameongeza kuwa, Maboresho mengine ni
pamoja na uwezo wa watoa huduma kuwarudia wateja kwa kuwapigia simu moja kwa
moja, kufanya ufuatiliaji wa masuala katika Mahakama yoyote nchini, pamoja na
kuwa rafiki zaidi kwa mtumiaji kwa kupunguza makosa ya kibinadamu.
Vilevile, Mahakama imeimarisha upatikanaji wa huduma
muda wote kwa kuanzisha Kituo cha Akiba cha Mfumo katika Mkoa wa Dar es Salaam,
ili kuhakikisha huduma hazikatiki hata kunapojitokeza changamoto za kiufundi.
Sambamba na hayo Mhe. Nkya amesisitiza kuwa, baada
ya mafunzo hayo, Mahakama inatarajia kuona ongezeko la ufanisi katika
kushughulikia mawasiliano ya wananchi, matumizi sahihi ya takwimu katika
kufanya maamuzi ya kiuendeshaji, pamoja na kuimarika kwa uwajibikaji na uwazi
kwa watumishi.
Msajili Mkuu, ametoa wito kwa washiriki wa mafunzo hayo kutumia maarifa watakayoyapata kuboresha huduma, kuimarisha maadili ya kazi na kuendelea kujenga imani ya wananchi kwa Mahakama.
Masajili
Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Eva Nkya akizungumza wakati alipokuwa
akifungua mafunzo kwa Maafisa Mirejesho wa Kituo cha Huduma kwa Mteja, leo 22 Januari, 2026 katika Ukumbi wa Chumba Maalumu cha Mifumo ya
Utoaji Taarifa (Judiciary Situation Room) kilichopo Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini
Dodoma.
Naibu Msajili na
Mkurugenzi wa Divisheni ya Ukaguzi wa Huduma za Kimahakama, Mirejesho kwa Umma
na Maadili, Mhe. Maira Kasonde akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha
Msajili Mkuu wa Mahakama ili kufungua mafunzo kwa Maafisa Mirejesho wa Kituo
cha Huduma kwa Mteja, leo 22, Januari, 2026 katika Chumba Maalumu cha Mifumo ya
Utoaji Taarifa (Judiciary Situation Room) kilichopo Makao Makuu ya Mahakama
jijini Dodoma.
Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Eva Nkya
(wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na sehemu ya Maafisa
Mirejesho wa Kituo cha Huduma kwa Mteja baada ya kufungua mafunzo kwa maafisa
hao, katika Chumba Maalumu cha Mifumo ya Utoaji Taarifa (Judiciary Situation
Room) Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma, wengine ni Naibu Msajili na
Mkurugenzi wa Divisheni ya Ukaguzi wa Huduma za Kimahakama, Mirejesho kwa umma
na Maadili, Mhe. Maira Kasonde wa kwanza kulia.
Sehemu nyingine ya maafisa mirejesho wa kituo cha huduma
kwa mteja wakiwa katika picha ya pamoja na Msajili Mkuu wa Mahakama Mhe. Eva
Nkya (wa kwanza kushoto) baada ya kufungua mafunzo kwa maafisa hayo katika
Chumba Maalumu cha Mifumo ya Utoaji Taarifa (Judiciary Situation Room) Makao Makuu
ya Mahakama jijini Dodoma, (wa pili kushoto) ni Naibu Msajili na Mkurugenzi wa
Divisheni ya Ukaguzi wa Huduma za Kimahakama, Mirejesho kwa umma na Maadili,
Mhe. Maira Kasonde.
Maafisa Mirejesho wa Kituo cha Huduma kwa Mteja
wakisikiliza hotuba ya Msajili Mkuu wa Mahakama Mhe. Eva Nkya (aliyesimama
mbele) wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa Maafisa Mirejesho wa Kituo cha Huduma
kwa Mteja, leo 22 Januari, 2026 katika Chumba Maalumu cha Mifumo ya Utoaji
Taarifa (Judiciary Situation Room) kilichopo Makao Makuu ya Mahakama jijini
Dodoma.
Sehemu ya Maafisa Mirejesho wa Kituo cha Huduma kwa Mteja wakifuatilia hotuba ya Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Eva Nkya (aliyesimama mbele)

.jpg)






Hakuna maoni:
Chapisha Maoni