Jumamosi, 7 Februari 2026

WATUMISHI SUMBAWANGA WAPATA MAFUNZO KUHUSU MAADILI KATIKA UTUMISHI WA UMMA

Na. Fredrick Mahava- Mahakama, Sumbawanga

Watumishi wa Mahakama Kanda ya Sumbawanga wamepata mafunzo juu ya Maadili katika utumishi wa Umma na mambo ya mchaka wa mtu mwenye uzoefu na maarifa kumsaidia mtu mwenye uzoefu mdogo kwa kumpa ushauri, muongozo, maarifa na msaada ili akue kielimu, kikazi au kimaisha (Mentorship) ambayo yalitolewa kwa njia mbili yaani uso kwa uso kwa waliokuwepo ukumbini na kwa njia ya Mtandao kwa waliokuwa mbali.

Mafunzo hayo yalifunguliwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Sumbawanga Mhe. Fredrick Manyanda jana tarehe 06 Februari 2026 ambayo yalifanyika katika Ukumbi wa Mahakama Kuu Sumbawanga.

Akizungumza wakati anafungua mafunzo hayo Mhe. Manyanda alisema, Kanda ya Sumbawanga imejiwekea utaratibu wa kufanya mafunzo kila Mwezi kwa watumishi ili kuwajengea uwezo na kuwafanya kuwa wabunifu zaidi katika kazi zao za kila siku.

Mafunzo hayo yalitolewa na wawezeshaji watatu ambao ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Sumbawanga Mhe, Joseph Luambano, Afisa Utumishi Mwandamizi Mahakama Kuu Sumbawanga Bi. Irene T. Mlangwa na Afisa Tawala Mahakama ya Hakimu Mkazi Rukwa Bi. Sarah C. Mwasomola ambao wasifu wao ulisomwa na msimamizi wa Mafunzo hayo Mhe. Elisha Mwasomola.

Mada ya Kwanza kuhusu Mentorship programu iliwasilishwa na Naibu Msajili Mahakama Kuu Sumbawanga Mhe. Joseph Luambano ambaye aliwataka watumishi wote wenye uzoefu wa kutosha kazini kuwa washauri (mentor) kwa wale ambao ndiyo wameajiriwa na hawana uzoefu kazini. Pia alielezea kuhusu misingi ya Maadili katika utumishi wa Umma na mambo ya mchaka wa mtu mwenye uzoefu na maarifa kumsaidia mtu mwenye uzoefu mdogo kwa kumpa ushauri, muongozo, maarifa na msaada ili akue kielimu, kikazi au kimaisha (Mentorship) kwa Maafisa wa Mahakama kwamba njia za kufanya Mentorship na Miongozo mbalimbali ya kufanya Mentorship.

Kwa upande wake, wakilishi wa mada ya pili Afisa Utumishi Mwandamizi Mahakama Kuu Sumbawanga Bi. Mlangwa na Afisa Tawala Mwandamizi Mahakama ya Hakimu Mkazi Rukwa Bi. Sarah ambao walifundisha kuhusu Maadili katika Utumishi wa Umma walisema ni muhimu kuzingatia miongozo, kanuni na taratibu zote za utumishi wa umma pale mtumishi unakuwa unamuhudumumia mwananchi ili kuondoa dukuduku la na aweze kupata majibu sahihi ya shida yake.

Aidha, Mhe. Manyanda wakati akichangi kuhusu mada zilizofundishwa alisema, suala la Mentorship sio tu kutoka kwa mkubwa kwenda kwa mdogo bali pia linaweza kuwa kutoka kwa mdogo kwenda kwa mkubwa.

Naye, Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Mhe. Thadeo Mwenempazi alisema kwenye suala ya Mentorship uhuru wa kujieleza unatakiwa kuwepo na utakuwa huru zaidi kama unafanya mambo yako kwa usahihi na hapo ndipo suala la maadili linapozingatiwa.

Wakati wa mafunzo hayo watumishi wa Mahakama Kanda ya Sumbawanga walipata wasaa wa kuuliza maswali mbalimbali kuhusu mada zilizowasilishwa na kupewa majibu ambayo yaliwasadia kuelewa zaidi.

Jaji mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Sumbawanga, Mhe. Fredrick Manyanda akifungua mafunzo kwa watumishi wa Mahakama Kanda ya sumbawanga juu ya Maadili katika utumishi wa Umma na Mentorship Programu

Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Mhe. Thadeo Mwenempazi akizungumza wakati wa mafunzo hayo

Naibu Msajili Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Mhe. Joseph Luambano akiwasilisha Mada wakati wa Mafunzo.

Sehemu ya Watumishi wa Mahakama Kanda ya Sumbawanga wakifuatilia kwa makini mafunzo yanayotolewa.

Afisa Tawala Mwandamizi Mahakama ya Hakimu Mkazi Rukwa Bi. Sarah C. Mwasomola akiwasilisha Mada wakati wa Mafunzo.

Afisa Utumishi Mwandamizi Mahakama Kuu Sumbawanga Bi. Irene T. Mlangwa akiwasilisha Mada wakati wa Mafunzo.

Mheshimiwa Elisha Mwasomola akitoa mwongozo wa Mafunzo kwa Watumishi Kanda ya Sumbawanga







Hakuna maoni:

Chapisha Maoni