Jumatano, 10 Mei 2017

KAIMU JAJI MKUU AENDELEA NA ZIARA YAKE KIKAZI MKOANI ARUSHA,AWEKA JIWE LA MSINGI-MAHAKAMA YA MWANZO KARATU


Jaji Mkuu wa Tanzania akiwa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Mhe. Theresia Mahongo wakifunua kitambaa kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi katika ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo, Karatu. Uwekaji wa jiwe hilo la msingi uliohudhuriwa na Watumishi wa Mahakama, Wananchi, Viongozi wa dini, Maafisa kutoka serikalini n.k, anayeshuhudia wa kwanza kulia ni Kaimu Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu, Kanda ya Arusha, Mhe. Sekela Moshi.
Ujenzi wa jengo jipya la Mahakama ya Mwanzo Karatu mjini ulianza mnamo Mwezi wa Novemba Mwaka 2012 kwa nguvu za wananchi kwa kuhamasishwa na Mkuu wa Wilaya pamoja na Hakimu wa Wilaya Mfawidhi. Aidha, thamani ya mradi huo wa umaliziaji wa jengo la Mahakama ya Mwanzo Karatu Mjini ni kiasi cha Fedha za Kitanzania Shilingi Milioni Mia Moja Thalathini na Saba Mia Mbili Sabini na Tano Elfu na Mia Tano Arobaini 137,275,540/=
Meza Kuu ikiwa katika hafla ya uwekaji jiwe la Msingi katika jengo jipya la Mahakama ya Mwanzo Karatu iliyopo mkoani Arusha.

Mhe. Kaimu Jaji Mkuu akitoa risala katika hafla hiyo fupi iliyohudhuriwa na wananchi wa mji wa Karatu, katika risala yake Mhe. Jaji Juma amewashukuru wananchi wa Wilaya hiyo kwa kujitoa kwa ujenzi wa Mahakama hiyo na kuwataka wananchi wengine kuwa na moyo huo ili Mahakama kwa kushirikiana na Wananchi kufikia azma ya kila kata kuwa na Mahakama ya Mwanzo.
Makundi mbalimbali ya wananchi walioshiriki katika hafla hiyo
Mhe. Kaimu Jaji Mkuu akikagua jengo la Mahakama ya Mwanzo Karatu aliloliwekea jiwe la msingi, mbele ni Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Mhe. Theresia Mahongo, mwenye tai nyekundu ni Hakimu Mkazi Mfawidhi, Mhe. Mukama. (picha na Mary Gwera, Karatu)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni