Na Evelina Odemba - Morogoro
Uongozi wa Chama cha Wanawake
Mahakimu na Majaji Tanzania (TAWJA) tarehe 8 Desemba 2021 umekabidhi kitabu katika
kituo Jumuishi cha Utoaji Haki cha Mahakama Kuu, Kanda ya Morogoro ili kuwasaidia
Majaji na Mahakimu kupata nukuu tofauti tofauti za kusimamia wakati wa kutekeleza
majukumu yao ya utoaji haki.
Kitabu hicho kilichozinduliwa
Ikulu hivi karibuni na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu
Hassan ikimepewa jina la “Gender Bench Book on Women’s Rights”
ambacho kinazungumzia masuala mbalimbali yanayomuhusu mwanamke upande wa sheria
pamoja na hukumu zilizotolewa kwenye mashauri yanayohusu mwanamke.
Akizungumza wakati wa kupokea
kitabu hicho, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Morogoro, Mhe. Paul
Ngwembe alitoa pongezi za dhati kwa TAWJA kwa kufanikisha kuandaa kitabu hicho muhimu
ambavyo kimesheheni ukweli unaopatikana katika jamii, huku akiongelea kuwa ukimpa
haki mwanamke ni sawa na kuipa haki jamii nzima.
Mhe. Ngwembe ambaye aliambata
na Jaji mwingine anayehudumu katika Kanda hiyo, Mhe. John Chaba aliongeza kwa
kusema kuwa “haki ya mwanamke ni haki ya jamii nzima” hivyo ni wajibu wa kila mmoja
kuhakikisha mwanamke anapatiwa haki stahiki.
Naye Kaimu Msajili Mahakama
Kuu, Kanda ya Morogoro, Mhe. Maua Hamduni aliongezea kwa kusema kuwa kitabu hicho
ni muhimu katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku na kitawarahisishia katika
uwajibikaji kwani kimezingatia nukuu mbalimbali za mashauri yaliyosikizwa na Majaji
waliootoa uamuzi ambao ni mwongozo ulio bora.
Akifafanua yaliyomo katika
kitabu hicho, Mratibu wa TAWJA ambaye pia ni Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo
Morogoro Mjini, Mhe. Adela Nyambele alisema kuwa kitabu kimechambua sheria
ambayo inamlinda mwanamke katika kila nyanja mbalimbali ikiwemo ajira, ndoa na hata
katika biashara na pia kiana uamuzi unaohusu mashauri juu ya unyanyasaji wa wanawake.
Kitabu cha Women’s
Access to Justice in Tanzania kinategemewa kugawaiwa kwa Majaji na Mahakimu wote
waliopo katika Kanda hiyo pia baadhi ya nakala zitawekwa kwenye Maktaba ya Mahakama
iliyopo ndani ya Jengo la Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki mkoani hapo ili mtu yeyote
mwenye uhitaji aweze kukisoma.
Jaji Mawidhi wa
Mahakama Kuu, Kanda ya Morogoro, Mhe Paul Ngwembe (katikati) pamoja na Mhe. John Chaba, Jaji mwingine anayehudumu katika
Kanfda hiyo (wa pili kulia) wakiwa na viongozi wa TAWJA baada ya kupokea kitabu
cha mwongozo wa mashauri.
Kaimu Msajili wa
Mahakama Kuu, Kanda ya Morogoro, Mhe. Maua Hamduni (wa tatu kutoka kushoto)
akipokea kitabu toka kwa mratibu wa TAWJA, Mhe. Adella Nyambele (kulia). Waliosimama
kushoto ni Mhe. Beatha Richard na Mhe Shida Nganga, ambao ni viongozi wa TAWJA
Kanda ya Morogoro walipotembelea Ofisi za Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki na
kugawa vitabu hivyo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni